وَكُلّٗا نَّقُصُّ عَلَيۡكَ مِنۡ أَنۢبَآءِ ٱلرُّسُلِ مَا نُثَبِّتُ بِهِۦ فُؤَادَكَۚ وَجَآءَكَ فِي هَٰذِهِ ٱلۡحَقُّ وَمَوۡعِظَةٞ وَذِكۡرَىٰ لِلۡمُؤۡمِنِينَ
Na yote tunayo kusimulia katika khabari za Mitume ni ya kukupa nguvu moyo wako. Na katika haya imekujia haki na mawaidha na ukumbusho kwa Waumini.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na tunakupa habari, ewe Mtume, za Mitume waliokuwa kabla yako zenye kila unalohitajia la kuupa nguvu moyo wako ya kusimama imara ili kubeba majukumu ya Utume. Na umekujia wewe, katika sura hii na hahabri zilizomo, ufafanuzi wa haki ambayo wewe uko juu yake. Na yamekujia wewe, katika hii sura, mawaidha ya kuwafanya makafiri wakomeke na ukumbusho wa kuwafanya wenye kumuamini Mwenyezi mungu na Mitume Wake wakumbuke.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس