قَالَ يَٰقَوۡمِ أَرَءَيۡتُمۡ إِن كُنتُ عَلَىٰ بَيِّنَةٖ مِّن رَّبِّي وَءَاتَىٰنِي رَحۡمَةٗ مِّنۡ عِندِهِۦ فَعُمِّيَتۡ عَلَيۡكُمۡ أَنُلۡزِمُكُمُوهَا وَأَنتُمۡ لَهَا كَٰرِهُونَ
Akasema: Enyi watu wangu! Hebu fikirini! Ikiwa mimi ninayo hoja wazi iliyo toka kwa Mola wangu Mlezi, na amenipa rehema kutoka kwake, nayo ikakufichikieni; je, tukulazimisheni kuikubali hali nyinyi mnaichukia?
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Nūḥ akasema, «Enyi watu wangu, iwapo mimi niko kwenye hoja iliyo wazi kutoka kwa Mola wangu katika yale niliyokuja nayo kutoka Kwake, itawafunukia nyinyi kwamba mimi niko kwenye haki inayotoka Kwake na kwamba Ameniletea rehema kutoka Kwake, nayo ni unabii na utume na kwamba Mwenyezi Mungu Amewafichia hayo kwa sababu ya ujinga wenu na kuhadaika kwenu. Basi je kwani inafaa niwalazimishe nayo kwa nguvu hali nyinyi mnaikanusha? Hatutafanya hivyo, lakini tunayategemeza mambo yenu kwa Mwenyezi Mungu ili Atoe uamuzi Anaoutaka kuhusu mambo yenu.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس