وَأُوحِيَ إِلَىٰ نُوحٍ أَنَّهُۥ لَن يُؤۡمِنَ مِن قَوۡمِكَ إِلَّا مَن قَدۡ ءَامَنَ فَلَا تَبۡتَئِسۡ بِمَا كَانُواْ يَفۡعَلُونَ
Na akafunuliwa Nuhu akaambiwa: Hataamini yeyote katika watu wako ila wale walio kwisha amini. Basi usisikitike kwa waliyo kuwa wakiyatenda.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na Mwenyezi Mungu, Aliyetakata na sifa za upungufu na kutukuka, Alimletea wahyi Nūḥ„ amani imshukiye, ilipolazimika adhabu juu ya watu wake kwamba hawatamuamini Mwenyezi Mungu isipokuwa walioamini kabla ya hapo, «basi usisikitike, ewe Nūḥ„ juu ya yale waliokuwa wakiyafanaya.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس