قَالُواْ يَٰهُودُ مَا جِئۡتَنَا بِبَيِّنَةٖ وَمَا نَحۡنُ بِتَارِكِيٓ ءَالِهَتِنَا عَن قَوۡلِكَ وَمَا نَحۡنُ لَكَ بِمُؤۡمِنِينَ
Wakasema: Ewe Hud! Hujatuletea dalili wazi. Wala sisi hatuiachi miungu yetu kwa kufuata kauli yako. Na wala sisi hatukuamini wewe.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Wakasema, «Ewe Hūd, hukutujia na hoja zilizo wazi juu ya usahihi wa yale unayotuitia. Na sisi si wenye kuwaacha waungu wetu tunaowaabudu kwa sababu ya maneno yako. Na sisi si wenye kukuamini wewe katika hilo unalolidai.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس