كَأَن لَّمۡ يَغۡنَوۡاْ فِيهَآۗ أَلَآ إِنَّ ثَمُودَاْ كَفَرُواْ رَبَّهُمۡۗ أَلَا بُعۡدٗا لِّثَمُودَ
Kama kwamba hawakuwako huko. Hebu zingatieni! Hakika kina Thamud walimkufuru Mola wao Mlezi. Hebu zingatieni! Thamud wamepotelea mbali!
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Kama kwamba wao, kwa haraka ya kuondoka kwao na kutoeka kwao, hawakuishi humo. Jueni mtanabahi kwamba Thamūd walikanusha aya za Mola wao na hoja Zake. Jueni mtanabahi kwamba kuwa mbali na kufukuzwa kwenye rehema ya Mwenyezi Mungu ni kwa hao Thamūd; ni upotevu ulioje na unyonge ulioje huo wao.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس