وَلَقَدۡ جَآءَتۡ رُسُلُنَآ إِبۡرَٰهِيمَ بِٱلۡبُشۡرَىٰ قَالُواْ سَلَٰمٗاۖ قَالَ سَلَٰمٞۖ فَمَا لَبِثَ أَن جَآءَ بِعِجۡلٍ حَنِيذٖ
Na wajumbe wetu walimjia Ibrahim kwa bishara njema, wakasema: Salama! Naye akasema: Salama! Hakukaa ila mara akaleta ndama wa kuchoma.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Hakika Malaika walimjia Ibrāhīm, amani imshukiye, wakimpa yeye na mke wake bishara ya Isḥḥḥaq na Ya'qūb baada yake, wakasema, «Salām (amani)» Akasema kuwarudishia maamkuzi yao, «Salām (amani)» Hapo akaondoka haraka na akrudi na mwanang>ombe wa kuchoma aliyenona ili wao wale.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس