وَٱمۡرَأَتُهُۥ قَآئِمَةٞ فَضَحِكَتۡ فَبَشَّرۡنَٰهَا بِإِسۡحَٰقَ وَمِن وَرَآءِ إِسۡحَٰقَ يَعۡقُوبَ
Na mkewe alikuwa kasimama wima, akacheka. Basi tukambashiria (kuzaliwa) Is-haq, na baada ya Is-haq Yaaqub.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na Sārah, mke wa Ibrāhīm, alikuwa amesimema nyuma ya pazia yuwasikia hayo maneno. Alicheka kwa kuyaonea ajabu aliyoyasikia. Hapo tukampa habari njema, kupitia kwa ndimi za Malaika, kwamba atazaa, kwa mume wake Ibrāhīm, mtoto atakayeitwa Isḥāq; na mtoto wake ataishi, na baada ya Isḥāq atakuwa na mjukuu kutoka kwake, naye ni Ya’qūb.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس