كَأَن لَّمۡ يَغۡنَوۡاْ فِيهَآۗ أَلَا بُعۡدٗا لِّمَدۡيَنَ كَمَا بَعِدَتۡ ثَمُودُ
Kama kwamba hawakuwamo humo. Zingatia walivyo angamia watu wa Madyana, kama walivyo angamia watu wa Thamud!
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Kama kwamba wao hawakukaa kwenye nyumba zao wakati wowote. Jueni kwamba watu wa Madyan waliepushwa na rehema ya Mwenyezi Mungu, kwa kuwa Mwenyezi Mungu aliwaangamiza watu wake na akawalaani, kama vile kina Thamūd walivyoepushwa na rehema Yake. Makabila mawili haya yalishirikiana katika kuwa mbali na rehema ya Mwenyezi Mungu na kuangamia.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس