يَوۡمَ يَدۡعُوكُمۡ فَتَسۡتَجِيبُونَ بِحَمۡدِهِۦ وَتَظُنُّونَ إِن لَّبِثۡتُمۡ إِلَّا قَلِيلٗا
Siku atakapo kuiteni, na nyinyi mkamuitikia kwa kumshukuru, na mkadhani kuwa hamkukaa ila muda mdogo tu.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Siku Atakapowaita Muumba wenu mtoke kwenye makaburi yenu na mkaitika amri ya Mwenyezi Munguna na mkaiyandama, na shukrani ni Zake kwa kila namna, na mkadhani, kwa kituko cha Siku ya Kiyama na kwa kipindi kirefu cha kukaa kwenu Akhera, kwamba nyinyi hamkukaa duniani isipokuwa muda mchache.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس