فَقُلۡنَا ٱذۡهَبَآ إِلَى ٱلۡقَوۡمِ ٱلَّذِينَ كَذَّبُواْ بِـَٔايَٰتِنَا فَدَمَّرۡنَٰهُمۡ تَدۡمِيرٗا
Tukawaambia: Nendeni kwa watu walio kanusha Ishara zetu. Basi tukawateketeza kabisa.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
na tukawaambia wao wawili,»Endeni kwa Fir’awn na watu wake waliozikanusha dalili za uola[7] wetu na uungu wetu.» Basi wakawaendea na wakawalingania wamuamini Mwenyezi Mungu, wamtii na wasimshirikishe. Wakawakanusha, na kwa hivyo tukawaangamiza maangamivu makubwa.
____________________
[7]Dalili ya uola wa Mwenyezi Mungu ni dalili ya kuwa yeye Ndiye Mola
____________________
[7]Dalili ya uola wa Mwenyezi Mungu ni dalili ya kuwa yeye Ndiye Mola
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس