وَٱلَّذِينَ إِذَا ذُكِّرُواْ بِـَٔايَٰتِ رَبِّهِمۡ لَمۡ يَخِرُّواْ عَلَيۡهَا صُمّٗا وَعُمۡيَانٗا
Na wale ambao wanapo kumbushwa Ishara za Mola wao Mlezi hawajifanyi viziwi nazo, na vipofu.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na ambao wakipewa mawaidha kwa aya za Qur’ani na dalili za upweke wa Mwenyezi Mungu hawajighafilishi nazo wakawa kama ambao ni viziwi hawakuzisikia na vipofu hawakuziona, lakini nyoyo zao zinazielewa na akili zao zinafunguka kuzikubali, na basi hapo wanajipomosha kwa Mwenyezi Mungu hali ya kusujudu na kutii.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس