وَسۡـَٔلۡ مَنۡ أَرۡسَلۡنَا مِن قَبۡلِكَ مِن رُّسُلِنَآ أَجَعَلۡنَا مِن دُونِ ٱلرَّحۡمَٰنِ ءَالِهَةٗ يُعۡبَدُونَ
Na waulize Mitume wetu tulio watuma kabla yako: Je! Tulifanya miungu mingine iabudiwe badala ya Rah'mani?
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na uwaulize, ewe Mtume, wafuasi wa wale tuliowatumiliza kabla yako miongoni mwa Mitume wetu na wabebaji sheria zao, «Je walikuja Mitume wao na ujumbe wa kuabudiwa asiyekuwa Mwenyezi Mungu?” Wao watakupasha habari kuwa hilo halikutukia, kwani Mitume wote walilingania kile ulichowaitia watu cha kumuabudu Mwenyezi Mungu, Peke Yake Asiye na mshirika, na wakakataza kuabudiwa asiyekuwa Mwenyezi Mungu.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس