قُلۡ إِنِّيٓ أَخَافُ إِنۡ عَصَيۡتُ رَبِّي عَذَابَ يَوۡمٍ عَظِيمٖ
Sema: Mimi naogopa adhabu ya Siku kubwa hiyo ikiwa nitamuasi Mola wangu Mlezi.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Sema, ewe Mtume, kuwaambia hawa wenye kumshirikisha Mwenyezi Mungu na asiyekuwa Yeye, «Mimi naogopa nikimuasi Mola wangu, nikaenda kinyume na maamrisho Yake, na nikamshirikisha Yeye na asiyekuwa Yeye, kuteremkiwa na adhabu kubwa Siku ya Kiyama.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس