ترجمة سورة الأعلى

Ali Muhsin Al - Swahili translation
ترجمة معاني سورة الأعلى باللغة السواحلية من كتاب Ali Muhsin Al - Swahili translation .

Al'A'alah


Litakase jina la Mola wako Mlezi aliye juu kabisa,

Aliye umba, na akaweka sawa,

Na ambaye amekadiria na akaongoa,

Na aliye otesha malisho,

Kisha akayafanya makavu, meusi.

Tutakusomesha wala hutasahau,

Ila akipenda Mwenyezi Mungu. Hakika Yeye anayajua yaliyo dhaahiri na yaliyo fichikana.

Na tutakusahilishia yawe mepesi.

Basi kumbusha, kama kukumbusha kunafaa.

Atakumbuka mwenye kuogopa.

Na atajitenga mbali nayo mpotovu,

Ambaye atauingia Moto mkubwa.

Tena humo hatakufa wala hawi hai.

Hakika amekwisha fanikiwa aliye jitakasa.

Na akakumbuka jina la Mola wake Mlezi, na akasali.

Lakini nyinyi mnakhiari maisha ya dunia!

Na Akhera ni bora na yenye kudumu zaidi.

Hakika haya yamo katika Vitabu vya mwanzo,

Vitabu vya Ibrahimu na Musa.
Icon