ترجمة معاني سورة النجم باللغة السواحلية من كتاب Ali Muhsin Al - Swahili translation
ﰡ
آية رقم 1
ﭑﭒﭓ
ﭔ
An-Najm
Naapa kwa nyota inapo tua,
آية رقم 2
ﭕﭖﭗﭘﭙ
ﭚ
Mwenzenu huyu hakupotea, wala hakukosea.
آية رقم 3
ﭛﭜﭝﭞ
ﭟ
Wala hatamki kwa matamanio.
آية رقم 4
ﭠﭡﭢﭣﭤ
ﭥ
Hayakuwa haya ila ni ufunuo ulio funuliwa;
آية رقم 5
ﭦﭧﭨ
ﭩ
Amemfundisha aliye mwingi wa nguvu,
آية رقم 6
ﭪﭫﭬ
ﭭ
Mwenye kutua, akatulia,
آية رقم 7
ﭮﭯﭰ
ﭱ
Naye yuko juu kabisa upeo wa macho.
آية رقم 8
ﭲﭳﭴ
ﭵ
Kisha akakaribia na akateremka.
آية رقم 9
ﭶﭷﭸﭹﭺ
ﭻ
Akawa ni kama baina ya mipinde miwili, au karibu zaidi.
آية رقم 10
ﭼﭽﭾﭿﮀ
ﮁ
Akamfunulia mja wake (Mwenyezi Mungu) alicho mfunulia.
آية رقم 11
ﮂﮃﮄﮅﮆ
ﮇ
Moyo haukusema uwongo uliyo yaona.
آية رقم 12
ﮈﮉﮊﮋ
ﮌ
Je! Mnabishana naye kwa aliyo yaona?
آية رقم 13
ﮍﮎﮏﮐ
ﮑ
Na akamwona mara nyingine,
آية رقم 14
ﮒﮓﮔ
ﮕ
Penye Mkunazi wa mwisho.
آية رقم 15
ﮖﮗﮘ
ﮙ
Karibu yake ndiyo ipo Bustani inayo kaliwa.
آية رقم 16
ﮚﮛﮜﮝﮞ
ﮟ
Kilipo ufunika huo Mkunazi hicho kilicho ufunuika.
آية رقم 17
ﮠﮡﮢﮣﮤ
ﮥ
Jicho halikuhangaika wala halikuruka mpaka.
آية رقم 18
ﮦﮧﮨﮩﮪﮫ
ﮬ
Kwa yakini aliona katika Ishara kubwa kabisa za Mola wake Mlezi.
آية رقم 19
ﮭﮮﮯ
ﮰ
Je! Mmemuona Lata na Uzza?
آية رقم 20
ﮱﯓﯔ
ﯕ
Na Manaat, mwingine wa tatu?
آية رقم 21
ﯖﯗﯘﯙ
ﯚ
Je! Nyinyi mnao wana wanaume na Yeye ndio awe na wanawake?
آية رقم 22
ﯛﯜﯝﯞ
ﯟ
Huo ni mgawanyo wa dhulma!
آية رقم 23
Hayo hayakuwa ila ni majina mliyo wapa nyinyi na baba zenu. Mwenyezi Mungu hakuleta uthibitisho wowote juu ya hayo. Hawafuati ila dhana tu na kipendacho nafsi. Na kwa yakini uwongofu ulikwisha wafikia kutoka kwa Mola wao Mlezi.
آية رقم 24
ﯼﯽﯾﯿ
ﰀ
Ati mtu anakipata kila anacho kitamani?
آية رقم 25
ﰁﰂﰃ
ﰄ
Mwenyezi Mungu tu ndiye Mwenye dunia na Akhera.
آية رقم 26
Na wako Malaika wangapi mbinguni, ambao uombezi wao hautafaa chochote isipo kuwa baada ya Mwenyezi Mungu kutoa idhini kwa amtakaye na kumridhia.
آية رقم 27
Hakika wasio amini Akhera bila ya shaka wao ndio wanawaita Malaika kwa majina ya kike.
آية رقم 28
Nao hawana ujuzi wowote kwa hayo isipo kuwa wanafuata dhana tu. Na dhana haisaidii chochote mbele ya haki.
آية رقم 29
Basi mwachilie mbali anaye upa kisogo ukumbusho wetu, na wala hataki ila maisha ya dunia.
آية رقم 30
Huo ndio mwisho wao wa ujuzi. Hakika Mola wako Mlezi ndiye anaye mjua zaidi mwenye kuipotea njia yake, na Yeye ndiye anaye mjua zaidi mwenye kuongoka.
آية رقم 31
Ni vya Mwenyezi Mungu vyote viliomo mbinguni na viliomo katika ardhi, ili awalipe walio tenda ubaya kwa waliyo yatenda, na walio tenda mema awalipe mema.
آية رقم 32
Ambao wanajiepusha na madhambi makuu na vitendo vichafu, isipo kuwa makosa khafifu. Hakika Mola wako Mlezi ni Mkunjufu wa maghfira, naye anakujueni sana tangu alipo kuumbeni kutoka kwenye ardhi, na mlipo kuwa mimba matumboni mwa mama zenu. Basi msijisifu usafi. Yeye anamjua sana mwenye kujikinga na maovu.
آية رقم 33
ﯢﯣﯤ
ﯥ
Je! Umemwona yule aliye geuka?
آية رقم 34
ﯦﯧﯨ
ﯩ
Na akatoa kidogo, kisha akajizuia?
آية رقم 35
ﯪﯫﯬﯭﯮ
ﯯ
Je! Anayo huyo ilimu ya ghaibu, basi ndio anaona?
آية رقم 36
Au hakuambiwa yaliyomo katika Vitabu vya Musa?
آية رقم 37
ﯸﯹﯺ
ﯻ
Na vya Ibrahimu aliye timiza ahadi?
آية رقم 38
ﯼﯽﯾﯿﰀ
ﰁ
Ya kwamba hakika nafsi iliyo beba madhambi haibebi madhambi ya mwengine?
آية رقم 39
ﰂﰃﰄﰅﰆﰇ
ﰈ
Na ya kwamba hatapata mtu ila aliyo yafanya mwenyewe?
آية رقم 40
ﰉﰊﰋﰌ
ﰍ
Na kwamba vitendo vyake vitaonekana?
آية رقم 41
ﰎﰏﰐﰑ
ﰒ
Kisha ndio atalipwa malipo yake kwa ukamilifu.
آية رقم 42
ﰓﰔﰕﰖ
ﰗ
Na kwamba kwao Mola wako Mlezi ndio mwisho.
آية رقم 43
ﰘﰙﰚﰛ
ﰜ
Na kwamba Yeye ndiye anaye leta kicheko na kilio.
آية رقم 44
ﰝﰞﰟﰠ
ﰡ
Na kwamba Yeye ndiye anaye fisha na kuhuisha.
آية رقم 45
ﭑﭒﭓﭔﭕ
ﭖ
Na kwamba Yeye ndiye aliye umba jozi, dume na jike
آية رقم 46
ﭗﭘﭙﭚ
ﭛ
Kutokana na mbegu ya uzazi inapo miminwa.
آية رقم 47
ﭜﭝﭞﭟ
ﭠ
Na kwamba ni juu yake ufufuo mwengine.
آية رقم 48
ﭡﭢﭣﭤ
ﭥ
Na kwamba ni Yeye ndiye anaye tosheleza na kukinaisha.
آية رقم 49
ﭦﭧﭨﭩ
ﭪ
Na kwamba hakika Yeye ndiye Mola Mlezi wa nyota ya Shii'ra.
آية رقم 50
ﭫﭬﭭﭮ
ﭯ
Na kwamba Yeye ndiye aliye waangamiza A'di wa kwanza,
آية رقم 51
ﭰﭱﭲ
ﭳ
Na Thamudi hakuwabakisha,
آية رقم 52
Na kabla yao kaumu ya Nuhu. Na hao hakika walikuwa ni madhaalimu zaidi, na waovu zaidi;
آية رقم 53
ﭿﮀ
ﮁ
Na miji iliyo pinduliwa, ni Yeye aliye ipindua.
آية رقم 54
ﮂﮃﮄ
ﮅ
Vikaifunika vilivyo funika.
آية رقم 55
ﮆﮇﮈﮉ
ﮊ
Basi neema gani ya Mola wako Mlezi unayo ifanyia shaka?
آية رقم 56
ﮋﮌﮍﮎﮏ
ﮐ
Hili ni Onyo katika maonyo yale yale ya zamani.
آية رقم 57
ﮑﮒ
ﮓ
Kiyama kimekaribia!
آية رقم 58
ﮔﮕﮖﮗﮘﮙ
ﮚ
Hapana wa kukifichua isipo kuwa Mwenyezi Mungu.
آية رقم 59
ﮛﮜﮝﮞ
ﮟ
Je! Mnayastaajabia maneno haya?
آية رقم 60
ﮠﮡﮢ
ﮣ
Na mnacheka, wala hamlii?
آية رقم 61
ﮤﮥ
ﮦ
Nanyi mmeghafilika?
آية رقم 62
ﮧﮨﮩﮪ
ﮫ
Basi msujudieni Mwenyezi Mungu, na mumuabudu.
تقدم القراءة