ترجمة معاني سورة النبأ باللغة السواحلية من كتاب Ali Muhsin Al - Swahili translation
ﰡ
آية رقم 1
ﭑﭒ
ﭓ
An-Naba'i
WANAULIZANA nini?
آية رقم 2
ﭔﭕﭖ
ﭗ
Ile khabari kuu,
آية رقم 3
ﭘﭙﭚﭛ
ﭜ
Ambayo kwayo wanakhitalifiana.
آية رقم 4
ﭝﭞ
ﭟ
La! Karibu watakuja jua.
آية رقم 5
ﭠﭡﭢ
ﭣ
Tena la! Karibu watakuja jua.
آية رقم 6
ﭤﭥﭦﭧ
ﭨ
Kwani hatukuifanya ardhi kama tandiko?
آية رقم 7
ﭩﭪ
ﭫ
Na milima kama vigingi?
آية رقم 8
ﭬﭭ
ﭮ
Na tukakuumbeni kwa jozi?
آية رقم 9
ﭯﭰﭱ
ﭲ
Na tukakufanya kulala kwenu ni mapumziko?
آية رقم 10
ﭳﭴﭵ
ﭶ
Na tukaufanya usiku ni nguo?
آية رقم 11
ﭷﭸﭹ
ﭺ
Na tukaufanya mchana ni wa kuchumia maisha?
آية رقم 12
ﭻﭼﭽﭾ
ﭿ
Na tukajenga juu yenu saba zenye nguvu?
آية رقم 13
ﮀﮁﮂ
ﮃ
Na tukaifanya taa yenye mwanga na joto;
آية رقم 14
ﮄﮅﮆﮇﮈ
ﮉ
Na tukateremsha maji yanayo anguka kwa kasi kutoka mawinguni,
آية رقم 15
ﮊﮋﮌﮍ
ﮎ
Ili tutoe kwayo nafaka na mimea,
آية رقم 16
ﮏﮐ
ﮑ
Na mabustani yenye miti iliyo kamatana.
آية رقم 17
ﮒﮓﮔﮕﮖ
ﮗ
Hakika siku ya uamuzi imewekewa wakati wake,
آية رقم 18
ﮘﮙﮚﮛﮜﮝ
ﮞ
Siku litapo pulizwa barugumu, nanyi mtakuja kwa makundi,
آية رقم 19
ﮟﮠﮡﮢ
ﮣ
Na mbingu zitafunguliwa, ziwe milango,
آية رقم 20
ﮤﮥﮦﮧ
ﮨ
Na milima itaondolewa na itakuwa kama sarabi.
آية رقم 21
ﮩﮪﮫﮬ
ﮭ
Hakika Jahannamu inangojea!
آية رقم 22
ﮮﮯ
ﮰ
Kwa walio asi ndio makaazi yao,
آية رقم 23
ﮱﯓﯔ
ﯕ
Wakae humo karne baada ya karne,
آية رقم 24
ﯖﯗﯘﯙﯚﯛ
ﯜ
Hawataonja humo chochote kibaridi wala kinywaji,
آية رقم 25
ﯝﯞﯟ
ﯠ
Ila maji yamoto sana na usaha,
آية رقم 26
ﯡﯢ
ﯣ
Ndio jaza muwafaka.
آية رقم 27
ﯤﯥﯦﯧﯨ
ﯩ
Hakika hao hawakuwa wakitaraji kuwa kuna hisabu.
آية رقم 28
ﯪﯫﯬ
ﯭ
Na wakikanusha Aya zetu kwa nguvu.
آية رقم 29
ﯮﯯﯰﯱ
ﯲ
Na kila kitu Sisi tumekidhibiti kwa kukiandika.
آية رقم 30
ﯳﯴﯵﯶﯷ
ﯸ
Basi onjeni! Nasi hatutakuzidishieni ila adhabu!
آية رقم 31
ﭑﭒﭓ
ﭔ
Hakika wachamngu wanastahiki kufuzu,
آية رقم 32
ﭕﭖ
ﭗ
Mabustani na mizabibu,
آية رقم 33
ﭘﭙ
ﭚ
Na wake walio lingana nao,
آية رقم 34
ﭛﭜ
ﭝ
Na bilauri zilizo jaa,
آية رقم 35
ﭞﭟﭠﭡﭢﭣ
ﭤ
Hawatasikia humo upuuzi wala uwongo -
آية رقم 36
ﭥﭦﭧﭨﭩ
ﭪ
Malipo kutoka kwa Mola wako Mlezi, kipawa cha kutosha.
آية رقم 37
Mola Mlezi wa mbingu na ardhi na vilio baina yao, Arrahman, Mwingi wa rehema; hawamiliki usemi mbele yake!
آية رقم 38
Siku atakapo simama Roho na Malaika kwa safu. Hawatasema ila Mwingi wa rehema aliye mruhusu, na atasema yaliyo sawa tu.
آية رقم 39
Hiyo ndiyo Siku ya haki. Basi anaye taka na ashike njia arejee kwa Mola wake Mlezi.
آية رقم 40
Hakika tumekuhadharisheni adhabu iliyo karibu kufika; Siku ambayo mtu atakapo ona yaliyo tangulizwa na mikono yake; na kafiri atasema: Laiti ningeli kuwa udongo!
تقدم القراءة