ترجمة معاني سورة النازعات باللغة السواحلية من كتاب Ali Muhsin Al - Swahili translation
ﰡ
آية رقم 1
ﮢﮣ
ﮤ
An-Nazi'at
Naapa kwa wanao komoa kwa nguvu,
آية رقم 2
ﮥﮦ
ﮧ
Na kwa wanao toa kwa upole,
آية رقم 3
ﮨﮩ
ﮪ
Na wanao ogelea,
آية رقم 4
ﮫﮬ
ﮭ
Wakishindana mbio,
آية رقم 5
ﮮﮯ
ﮰ
Wakidabiri mambo.
آية رقم 6
ﮱﯓﯔ
ﯕ
Siku kitapo tetemeka cha kutetemeka,
آية رقم 7
ﯖﯗ
ﯘ
Kifuate cha kufuatia.
آية رقم 8
ﯙﯚﯛ
ﯜ
Siku hiyo nyoyo zitapiga piga,
آية رقم 9
ﯝﯞ
ﯟ
Macho yatainama chini.
آية رقم 10
ﯠﯡﯢﯣﯤ
ﯥ
Sasa wanasema: Ati kweli tutarudishwa kwenye hali ya kwanza?
آية رقم 11
ﯦﯧﯨﯩ
ﯪ
Hata tukiwa mifupa iliyo bunguliwa?
آية رقم 12
ﯫﯬﯭﯮﯯ
ﯰ
Wanasema: Basi marejeo hayo ni yenye khasara!
آية رقم 13
ﯱﯲﯳﯴ
ﯵ
Kwa hakika hayo ni ukelele mmoja tu,
آية رقم 14
ﯶﯷﯸ
ﯹ
Mara watakuwa kwenye uwanda wa mkutano!
آية رقم 15
ﯺﯻﯼﯽ
ﯾ
Je! Imekufikia hadithi ya Musa?
آية رقم 16
ﯿﰀﰁﰂﰃﰄ
ﰅ
Mola wake Mlezi alipo mwita katika bonde takatifu la T'uwaa, akamwambia:
آية رقم 17
ﭑﭒﭓﭔﭕ
ﭖ
Nenda kwa Firauni. Hakika yeye amezidi jeuri.
آية رقم 18
ﭗﭘﭙﭚﭛﭜ
ﭝ
Umwambie: Je! Unapenda kujitakasa?
آية رقم 19
ﭞﭟﭠﭡ
ﭢ
Nami nitakuongoa ufike kwa Mola wako Mlezi, upate kumcha.
آية رقم 20
ﭣﭤﭥ
ﭦ
Basi alimwonyesha Ishara kubwa.
آية رقم 21
ﭧﭨ
ﭩ
Lakini aliikadhibisha na akaasi.
آية رقم 22
ﭪﭫﭬ
ﭭ
Kisha alirudi nyuma, akaingia kufanya juhudi.
آية رقم 23
ﭮﭯ
ﭰ
Akakusanya watu akanadi.
آية رقم 24
ﭱﭲﭳﭴ
ﭵ
Akasema: Mimi ndiye Mola wenu Mlezi mkuu kabisa.
آية رقم 25
ﭶﭷﭸﭹﭺ
ﭻ
Basi hapo Mwenyezi Mungu akamshika kumuadhibu kwa la mwisho na la mwanzo.
آية رقم 26
ﭼﭽﭾﭿﮀﮁ
ﮂ
Kwa hakika katika haya yapo mazingatio kwa wanao ogopa.
آية رقم 27
Je! Ni vigumu zaidi kukuumbeni nyinyi au mbingu? Yeye ndiye aliye ijenga!
آية رقم 28
ﮋﮌﮍ
ﮎ
Akainua kimo chake, na akaitengeneza vizuri.
آية رقم 29
ﮏﮐﮑﮒ
ﮓ
Na akautia giza usiku wake, na akautokeza mchana wake.
آية رقم 30
ﮔﮕﮖﮗ
ﮘ
Na juu ya hivyo ameitandaza ardhi.
آية رقم 31
ﮙﮚﮛﮜ
ﮝ
Akatoa ndani yake maji yake na malisho yake,
آية رقم 32
ﮞﮟ
ﮠ
Na milima akaisimamisha,
آية رقم 33
ﮡﮢﮣ
ﮤ
Kwa nafuu yenu na mifugo yenu.
آية رقم 34
ﮥﮦﮧﮨ
ﮩ
Basi itakapo fika hiyo balaa kubwa,
آية رقم 35
ﮪﮫﮬﮭﮮ
ﮯ
Siku ambayo mtu atakumbuka aliyo yafanya,
آية رقم 36
ﮰﮱﯓﯔ
ﯕ
Na Jahannamu itadhihirishwa kwa mwenye kuona,
آية رقم 37
ﯖﯗﯘ
ﯙ
Basi ama yule aliye zidi ujeuri,
آية رقم 38
ﯚﯛﯜ
ﯝ
Na akakhiari maisha ya dunia,
آية رقم 39
ﯞﯟﯠﯡ
ﯢ
Kwa hakika Jahannamu ndiyo makaazi yake!
آية رقم 40
Na ama yule anaye ogopa kusimamishwa mbele ya Mola wake Mlezi, na akajizuilia nafsi yake na matamanio,
آية رقم 41
ﯭﯮﯯﯰ
ﯱ
Basi huyo, Pepo itakuwa ndiyo makaazi yake!
آية رقم 42
ﯲﯳﯴﯵﯶ
ﯷ
Wanakuuliza Saa (ya Kiyama) itakuwa lini?
آية رقم 43
ﯸﯹﯺﯻ
ﯼ
Una nini wewe hata uitaje?
آية رقم 44
ﯽﯾﯿ
ﰀ
Kwa Mola wako Mlezi ndio mwisho wake.
آية رقم 45
ﰁﰂﰃﰄﰅ
ﰆ
Kwa hakika wewe ni mwonyaji tu kwa mwenye kuikhofu.
آية رقم 46
Ni kama kwamba wao siku watapo iona (hiyo Saa) hawakukaa ila jioni moja tu, au mchana wake.
تقدم القراءة