ترجمة معاني سورة النازعات باللغة السواحلية من كتاب الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس
ﰡ
آية رقم 1
ﮢﮣ
ﮤ
Anaapa Mwenyezi Mungu kwa Malaika ambao huzing’oa roho za makafiri mng’oo mkali.
آية رقم 2
ﮥﮦ
ﮧ
Na kwa Malaika ambao huzitukua roho za Waumini kwa uchangamfu na upole.
آية رقم 3
ﮨﮩ
ﮪ
Na kwa Malaika wanaoogelea katika kushuka kwao kutoka mbinguni na kupaa kwao kwenda mbinguni.
آية رقم 4
ﮫﮬ
ﮭ
Na kwa Mlaika ambao wanakimbilia kutekeleza amri za Mwenyezi Mungu.
آية رقم 5
ﮮﮯ
ﮰ
Na kwa Malaika wanaopitisha amri za Mola wao katika mambo ya ulimwengu waliowakilishwa kuyafanya na kuyasimamia, - Wala haifai kwa kiumbe kukiapia chochote kile, bali yapasa kiapo chake kiwe ni kwa jina la Mola wake Muumba au sifa Zake. Na lau ataapa kwa asiye Muumba wake, basi huyo amekuwa mshirikina - Watafufuliwa viumbe bila shaka na watahesabiwa.
آية رقم 6
ﮱﯓﯔ
ﯕ
Siku ambayo ardhi itatetemeka kwa mvuvuo wa kwanza:
آية رقم 7
ﯖﯗ
ﯘ
mvuvio wa kufisha, ukifuatiwa na mvuvio mwingine wa kuhuisha.
آية رقم 8
ﯙﯚﯛ
ﯜ
Nyoyo za makafiri, Siku hiyo, zitakuwa na papatiko kwa kicho kikubwa.
آية رقم 9
ﯝﯞ
ﯟ
Macho ya makafiri hao yatakuwa madhalilifu kwa kitisho watakachokiona.
آية رقم 10
ﯠﯡﯢﯣﯤ
ﯥ
Wanasema hawa wakanushao kufufuliwa:
آية رقم 11
ﯦﯧﯨﯩ
ﯪ
«Je, tutarudishwa baada ya kufa kwetu kwenye yale tuliyokuwa nayo katika ardhi? Je, tutarudishwa na hali tushakuwa mifupa iliochakaa?»
آية رقم 12
ﯫﯬﯭﯮﯯ
ﯰ
Wakasema: «Kurejea kwetu huko kutakuwa kutupu kusikokuwa kweli.’
آية رقم 13
ﯱﯲﯳﯴ
ﯵ
Hakika tukio hilo litakuwa kwa mvivio mmoja tu.
آية رقم 14
ﯶﯷﯸ
ﯹ
Wakitahamaki wao wako hai juu ya ardhi baada ya kuwa walikuwa ndani yake.
آية رقم 15
ﯺﯻﯼﯽ
ﯾ
Je imekujilia, ewe Mtume, habari ya Mūsā?
آية رقم 16
ﯿﰀﰁﰂﰃﰄ
ﰅ
Pindi Mola wake Alipomwita katika bonde lililotakaswa na kubarikiwa, la Ṭuwā. Akamwambia:
آية رقم 17
ﭑﭒﭓﭔﭕ
ﭖ
«Enda kwa Firauni. Hakika yeye amekiuka mno katika kuasi.
آية رقم 18
ﭗﭘﭙﭚﭛﭜ
ﭝ
Ukamwambie, ‘Je, unapendelea kuitakasa nafsi yako na upungufu na kuipamba na imani?
آية رقم 19
ﭞﭟﭠﭡ
ﭢ
Na nikuelekeze njia ya kumtii Mola wako, upate kumcha na kumuogopa?’»
آية رقم 20
ﭣﭤﭥ
ﭦ
Mūsā alimuonyesha Firauni alama kubwa: fimbo na mkono.
آية رقم 21
ﭧﭨ
ﭩ
Hapo Firauni alimkanusha Nabii wa Mwenyezi Mungu , naye ni Mtume Mūsā, amani imshukie, na alimuasi Mola wake Aliyetukuka.
آية رقم 22
ﭪﭫﭬ
ﭭ
Kisha alikengeuka hali ya kuipa mgongo Imani na kufanya bidii katika kumpinga Mūsā.
آية رقم 23
ﭮﭯ
ﭰ
Hapo aliwakusanya raia wa utawala wake na akawaita kwa
آية رقم 24
ﭱﭲﭳﭴ
ﭵ
kuwaambia,»Mimi ndiye mola wenu ambaye hakuna mola mwengine aliye juu yake.»
آية رقم 25
ﭶﭷﭸﭹﭺ
ﭻ
Hapo Mwenyezi Mungu Alimtesa kwa adhabu ya duniani na ya Akhera.
آية رقم 26
ﭼﭽﭾﭿﮀﮁ
ﮂ
Na Akaifanya adhabu hiyo iwe ni mazingatio na ni onyo kwa watu mfano wake kati ya wale waasi. Hakika Firauni na kile kilichompata cha adhabu ni mawaidha kwa mwenye kuwaidhika na kutishika.
آية رقم 27
Je, kufufuliwa kwenu, enyi watu, baada ya kufa ni kugumu zaidi, katika vipimo vyenu, au ni kuumbwa kwa mbingu?
آية رقم 28
ﮋﮌﮍ
ﮎ
Amezipanga juu yenu kama jengo. Na Ameinua sakafu yake angani, haina tofauti wala nyufa.
آية رقم 29
ﮏﮐﮑﮒ
ﮓ
Na Ameutia giza usiku wake kwa kutwa kwa jua lake. Na Ameweka wazi mchana wake kwa kuchomoza kwake.
آية رقم 30
ﮔﮕﮖﮗ
ﮘ
Na ardhi baada ya kuumba mbingu Ameitandaza. Na Ameweka humo manufaa yake.
آية رقم 31
ﮙﮚﮛﮜ
ﮝ
Na Ametumbua humo chemchemu za maji. Na Ameotesha humo mimea inayolishwa.
آية رقم 32
ﮞﮟ
ﮠ
Na Ameyakita humo majabali yakiwa ni vigingi vyake. Ameumba, Aliyetakasika na kila upungufu,
آية رقم 33
ﮡﮢﮣ
ﮤ
neema zote hizi zikiwa ni manufaa kwenu na kwa wanyama wenu. (Hakika kurudisha kuumbwa kwenu, Siku ya Kiyama, ni sahali kwa Mwenyezi Mungu kushinda kuumba viumbe hivyo vyingine. Na vyote hivyo, kwa Mwenyezi Mungu, ni rahisi na ni vipesi).
آية رقم 34
ﮥﮦﮧﮨ
ﮩ
Pindi kitakapokuja Kiyama Kikubwa na balaa nzito, nao ni Mvuvio wa pili. Kipindi hicho zitaoneshwa kwa binadamu vitendo vyake vyote, za kheri na za shari.
آية رقم 35
ﮪﮫﮬﮭﮮ
ﮯ
Hapo atazikumbuka na kuzitambua.
آية رقم 36
ﮰﮱﯓﯔ
ﯕ
Na utaoneshwa Moto wa Jahanamu kwa kila aonaye, uwe waonekana waziwazi.
آية رقم 37
ﯖﯗﯘ
ﯙ
Ama yule atakayekiuka amri ya Mwenyezi Mungu
آية رقم 38
ﯚﯛﯜ
ﯝ
na akapendelea maisha ya ulimwenguni kuliko ya Akhera,
آية رقم 39
ﯞﯟﯠﯡ
ﯢ
basi kwa kweli marejeo yake ni Motoni.
آية رقم 40
Na ama yule atakayeogopa kusimama mbele ya Mwenyezi Mungu kuhesabiwa na akaikanya nafsi yake na matamanio mapotofu,
آية رقم 41
ﯭﯮﯯﯰ
ﯱ
basi Peponi ndiko makazi yake.
آية رقم 42
ﯲﯳﯴﯵﯶ
ﯷ
Wanakuuliza washirikina, ewe Mtume, kwa madharau, kuhusu wakati wa kuanzia Kiyama unachowaonya.
آية رقم 43
ﯸﯹﯺﯻ
ﯼ
Wewe huna kamwe ujuzi nacho.
آية رقم 44
ﯽﯾﯿ
ﰀ
Bali mambo ya ujuzi huo yarejeshwe kwa Mwenyezi Mungu, Mwenye Sifa Tukufu.
آية رقم 45
ﰁﰂﰃﰄﰅ
ﰆ
Wewe linalokuhusu katika habari zake ni kumuonya nacho yule anayekiogopa.
آية رقم 46
Kama kwamba wao siku watakapouona Kiyama kimesimama, watakuwa hawakukaa katika maisha yao ya duniani, kwa vituko vya hiko Kiyama, isipokuwa ni kama kwamba wamkaa kati ya adhuhuri mpaka kutwa juwa, au ni kama kati ya kuchomoza jua mpaka nusu ya mchana.
تقدم القراءة