ترجمة معاني سورة الواقعة باللغة السواحلية من كتاب الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس

الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس

آية رقم 2
Hakutakuwa na yoyote mwenye kukanusha kusimama kwake.
آية رقم 3
Ni chenye kuwainamisha chini maadui wa Mwenyezi Mungu ndani ya Moto na ni chenye kuwainua juu Peponi wale wenye kumtegemea.
آية رقم 5
Na yakamumunyuliwa majabali mmumunyuo wa kina.
آية رقم 6
Yakawa vumbi lenye kuruka angani lililosukumwa na upepo.
آية رقم 8
Kundi la watu wa upande wa kulia, wenye daraja kubwa. Ni kikubwa kilioje cheo chao!
آية رقم 9
Kuna na kundi la watu wa upande wa kushoto, wenye daraja duni. Ni mbaya iliyoje hali yao!
آية رقم 10
Na wale waliotangulia mbele kwenye kheri duniani ndio wenye kutangulia mbele kwenye daraja za juu huko Akhera.
آية رقم 11
Wao ndio walioletwa karibu kwa Mwenyezi Mungu,
آية رقم 12
Mola wao Atawatia kwenye mabustani ya Pepo ya starehe.
آية رقم 13
Watayaingia watu wengi watu wa mwanzo wa ummah huu, na ummah wengineo wasiokuwa wao,
آية رقم 14
na wachache miongoni mwa watu mwisho wa ummah huu,
آية رقم 15
wakiwa juu ya vitanda vilivyofumwa kwa dhahabu,
آية رقم 16
na wakiwa katika hali ya kuvitegemea na huku wanaelekeana na kukutana.
آية رقم 17
Wanawazunguka wao kuwatumikia watumishi vijana wasiozeeka wala kufa,
آية رقم 18
wakiwa na vikombe, mabirika na gilasi kutoka kwenye chemchemi ya pombe yenye kupita ndani ya Pepo,
آية رقم 20
Na watawazunguka wao watumishi vijana na kila kitu wanachokichagua miongoni mwa matunda,
آية رقم 22
Na watakuwa na wanawake wenye macho makubwa kama kwamba wao,
آية رقم 23
kwa usafi wao na uzuri wao, ni lulu iliyohifadhiwa ndani ya mashaza yake,
آية رقم 24
hali hayo yakiwa ni malipo yao kwa yale waliokuwa wakiyafanya duniani.
آية رقم 25
Hawatasikia humo Peponi ubatilifu wala yale ya kuwatia madhambini kuyasikia,
آية رقم 26
isipokuwa maneno yasiyokuwa na kasoro hizi na kusalimiana wao kwa wao.
آية رقم 28
ni kikubwa kilioje cheo chao na malipo yao!
آية رقم 29
Watakuwa kwenye mikunazi isiyo na miba, na ndizi zilizopandana na kupangika,
آية رقم 30
kila ndizi juu ya nyingine, na vivuli vya daima visivyoondoka,
آية رقم 31
na maji yanayotembea yasiyokatika,
آية رقم 33
yasiyomalizika wala kuwaishia wala hakuna kizuizi chochote kinachowazuia wao kuyafikia,
آية رقم 34
na matandiko yaliyoinuliwa juu ya vitanda.
آية رقم 35
Sisi tumewaumba wanawake wa watu wa Peponi umbile ambalo silo lile umbile lililokuwa duniani, umbile lililokamilika lisilokubali kutoweka,
آية رقم 36
na tumewafanya ni wanawali wenye kujipendekeza kwa waume zao,
آية رقم 37
hali ya kuwa ni marika na wao kimiaka.
آية رقم 38
Tumewaumbia wanawake hao watu wa upande wa kulia.
آية رقم 41
Na watu wa upande wa kushoto, ni mbaya iliyoje hali yao na malipo yao!
آية رقم 42
Watakuwa kwenye upepo ulio moto utokanao na joto la Moto wa Jahanamu utakaozuia pumzi zao, na maji moto yanayochemka,
آية رقم 45
Kwani wao walikuwa duniani wakijistarehesha kwa vitu vya haramu wakijiepusha na yale ambayo Mitume walikuja nayo.
آية رقم 46
Na walikuwa wamesimama wima katika kumkanusha Mwenyezi Mungu na kumshirikisha na kumuasi, na hawakuwa na nia ya kutubia kwa hayo.
Na walikuwa wakisema hali ya kukanusha Ufufuzi, «Je hivi sisi tutafufuliwa tutakapokufa na tukawa mchanga na mifupa iliyochakaa?» Maneno yao hayo yanaonesha kuwa wao walikuwa wakiliona jambo hili la kufufuliwa kuwa liko mbali na ukweli na wakilikanusha.
آية رقم 48
«Je tutafufuliwa sisi na hali baba zetu waliotangulia wamekuwa mchanga uliotapakaa kwenye ardhi?»
آية رقم 49
Sema uwaambie, «Hakika wa mwanzo na wa mwisho miongoni mwa binadamu
آية رقم 50
watakusanywa katika Siku iliyowekewa wakati maalumu, nayo ni Siku ya Kiyama.
آية رقم 51
«Kisha nyinyi, enyi mliopotea njia ya uongofu mnaokanusha onyo la Mwenyezi Mungu na agizo Lake,
آية رقم 53
nao ni katika miti mibaya zaidi, na ni wenye kujaza matumbo yenu kutokana nao kwa sababu ya ukali wa njaa,
آية رقم 54
na ni wenye kunywa juu yake maji yaliyo moto hadi ya mwisho, yasiyomaliza kiu.
آية رقم 55
Mtayanywa maji hayo kwa wingi kama vile ngamia wenye kiu wasioshiba maji kwa ugonjwa uliowapata.»
آية رقم 56
Adhabu hii watakayoipata ndiyo zawadi Aliyowaandalia Siku ya Kiyama. Katika haya kuna kuwalaumu na kuwacheza shere.
آية رقم 57
Sisi tumewaumba, enyi watu, na hamkuwa kitu chochote. Basi si msadiki kuwa kuna kufufuliwa?
آية رقم 58
Mnayaonaje maji ya manii mnayoyatupa ndani ya vizazi vya wake zenu,
آية رقم 59
je nyinyi ndio mnaomuumba mwanadamu kutokana na hayo au ni sisi ndio wenye kuumba?
آية رقم 62
Na hakika mlijua kuwa Mwenyezi Mungu Aliwaumba uumbaji wa kwanza na hamkuwa kitu chochote. Basi si mkumbuke uweza wa Mwenyezi Mungu wa kuwaumba mara nyingine?
آية رقم 64
Je ni nyinyi mnaoziotesha kutoka ardhini? Sisi ndio tuaozituliza na kuziotesha ardhini.
آية رقم 65
Lau tungalitaka tungaliifanya mimea inayotokana na mbegu hizo kuwa mapepe, haimkiniki kunufaika nayo kwa kula,
آية رقم 66
mkawa mnaona ajabu kwa kilichoshukia mimea yenu na mnasema, «Sisi tumepata hasara na ni wenye kuungulika.
آية رقم 69
Je ni nyinyi mliyoyateremsha kutoka kwenye mawingu hadi kwenye kituo cha ardhi au ni sisi tuliyoyateremsha ili kuwarehemu nyinyi?
آية رقم 70
Lau tungalitaka tungaliyafanya maji haya yawe na chumvi sana, ikiwa haiwezekani kunufaika nayo kwa kunywa wala kwa mimea. Basi si mumshukuru Mola wenu kwa kuteremsha maji tamu kwa kuwanufaisha nyinyi.
آية رقم 72
Je ni nyinyi mlioufanya mti wake, unaozalisha moto kwa kukwaruzwa, upatikane au ni sisi tulioufanya upatikane?
آية رقم 73
Sisi tumeufanya moto wenu mnaouwasha ni ukumbusho kwenu wa Moto wa Jahanamu na pia ni manufaa kwa wasafiri.
آية رقم 74
Basi mtakase Mola wako, ewe Nabii, Aliye mtukufu Mwenye ukamilifu wa majina na sifa, Mwingi wa wema na kheri.
آية رقم 75
Mwenyezi Mungu Anaapa kwa mapomoko ya nyota nyakati za kuzama kwake mbinguni.
آية رقم 77
Hakika hii Qur’ani iliyoteremshiwa Muhammad ni Qur’ani yenye manufaa makubwa, yenye kheri nyingi na yenye elimu tele,
آية رقم 78
iliyo ndani ya Kitabu kilichohifadhiwa, kilichofichwa na macho ya viumbe, nacho ni Kitabu ambacho kiko mikononi mwa Malaika.
آية رقم 79
Hawaigusi Qur’ani isipokuwa malaika watukufu ambao Mwenyezi Mungu Amewasafisha na aibu na madhambi. Na pia hawaigusi isipokuwa watu waliojitohirisha na ushirikina na janaba na ukosefu wa udhu.
آية رقم 80
Na hii Qur’ani tukufu imeteremshwa kutoka kwa Mola wa viumbe vyote, kwani hiyo ndiyo haki isiyo na shaka ndani yake.
آية رقم 82
Na je mnaifanya shukrani yenu kwa neema za Mola wenu ni kuwa nyinyi mnazikanusha na kukufuru? Hapa pana makaripio kwa anayedharau amri za Qur’ani na kutojali mwito wake.
آية رقم 83
Basi je mnaweza pindi roho ya mmoja wenu inapofika kwenye koo katika uchungu wa kifo,
آية رقم 84
na hali nyinyi mmehudhuria mnamtazama, kuizuia roho yake ndani ya mwili wake? Hamtaweza hilo!
آية رقم 85
Na sisi tuko karibu na yeye zaidi, kupitia Malaika wetu, kuliko nyinyi, lakini nyinyi hamuwaoni.
آية رقم 86
Na je mnaweza, iwapo nyinyi si wenye kuhesabiwa wala kulipwa kwa matendo yenu,
آية رقم 87
kuirudisha roho kwenye mwili, iwapo nyinyi ni wakweli? Hamtaweza kuirudisha.
آية رقم 88
Basi iwapo yule anayekufa ni kati ya watu wa upande wa kulia, atapata rehema kunjufu na furaha,
آية رقم 89
wakati wa kufa kwake, na kila kinachoifurahisha nafsi yake, Na atapata Pepo ya starehe huko Akhera.
آية رقم 91
ataambiwa, «Umesalimika na kuwa kwenye amani, kwa kuwa wewe ni miongoni mwa watu wa upande wa kulia.»
آية رقم 92
Na iwapo yule anayekufa ni miongoni mwa wenye kukanusha kufufuliwa, waliopotoka na njia ya uongofu,
آية رقم 93
basi atapata makaribisho ya kinywaji cha moto wa Jahanamu kilichochemshwa, kilicho na joto hadi ya mwisho,
آية رقم 94
na atachomwa na Moto na aungulike na adhabu yake kali.
آية رقم 95
Hakika habari hii tumezokuelezea, ewe Mtume, ni ukweli wa yakini usio na shaka.
آية رقم 96
Basi litakase jina la Mola wako Aliyetukuka na umtakase na yale ambayo madhalimu na wenye kukanusha wanayasema. Mwenyezi Mungu Yuko juu ya yale wanayoyasema ujuu mkubwa sana.
تقدم القراءة