ترجمة معاني سورة الحديد باللغة السواحلية من كتاب الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس
الترجمة الإنجليزية - صحيح انترناشونال
المنتدى الإسلامي
الترجمة الإنجليزية
الترجمة الفرنسية - المنتدى الإسلامي
نبيل رضوان
الترجمة الإسبانية
محمد عيسى غارسيا
الترجمة الإسبانية - المنتدى الإسلامي
الترجمة الإسبانية (أمريكا اللاتينية) - المنتدى الإسلامي
المنتدى الإسلامي
الترجمة البرتغالية
حلمي نصر
الترجمة الألمانية - بوبنهايم
عبد الله الصامت
الترجمة الألمانية - أبو رضا
أبو رضا محمد بن أحمد بن رسول
الترجمة الإيطالية
عثمان الشريف
الترجمة التركية - مركز رواد الترجمة
فريق مركز رواد الترجمة بالتعاون مع موقع دار الإسلام
الترجمة التركية - شعبان بريتش
شعبان بريتش
الترجمة التركية - مجمع الملك فهد
مجموعة من العلماء
الترجمة الإندونيسية - شركة سابق
شركة سابق
الترجمة الإندونيسية - المجمع
وزارة الشؤون الإسلامية الأندونيسية
الترجمة الإندونيسية - وزارة الشؤون الإسلامية
وزارة الشؤون الإسلامية الأندونيسية
الترجمة الفلبينية (تجالوج)
مركز رواد الترجمة بالتعاون مع موقع دار الإسلام
الترجمة الفارسية - دار الإسلام
فريق عمل اللغة الفارسية بموقع دار الإسلام
الترجمة الفارسية - حسين تاجي
حسين تاجي كله داري
الترجمة الأردية
محمد إبراهيم جوناكري
الترجمة البنغالية
أبو بكر محمد زكريا
الترجمة الكردية
حمد صالح باموكي
الترجمة البشتوية
زكريا عبد السلام
الترجمة البوسنية - كوركت
بسيم كوركورت
الترجمة البوسنية - ميهانوفيتش
محمد مهانوفيتش
الترجمة الألبانية
حسن ناهي
الترجمة الأوكرانية
ميخائيلو يعقوبوفيتش
الترجمة الصينية
محمد مكين الصيني
الترجمة الأويغورية
محمد صالح
الترجمة اليابانية
روايتشي ميتا
الترجمة الكورية
حامد تشوي
الترجمة الفيتنامية
حسن عبد الكريم
الترجمة الكازاخية - مجمع الملك فهد
خليفة الطاي
الترجمة الكازاخية - جمعية خليفة ألطاي
جمعية خليفة الطاي الخيرية
الترجمة الأوزبكية - علاء الدين منصور
علاء الدين منصور
الترجمة الأوزبكية - محمد صادق
محمد صادق محمد
الترجمة الأذرية
علي خان موساييف
الترجمة الطاجيكية - عارفي
فريق متخصص مكلف من مركز رواد الترجمة بالشراكة مع موقع دار الإسلام
الترجمة الطاجيكية
خوجه ميروف خوجه مير
الترجمة الهندية
مولانا عزيز الحق العمري
الترجمة المليبارية
عبد الحميد حيدر المدني
الترجمة الغوجراتية
رابيلا العُمري
الترجمة الماراتية
محمد شفيع أنصاري
الترجمة التلجوية
مولانا عبد الرحيم بن محمد
الترجمة التاميلية
عبد الحميد الباقوي
الترجمة السنهالية
فريق مركز رواد الترجمة بالتعاون مع موقع دار الإسلام
الترجمة الأسامية
رفيق الإسلام حبيب الرحمن
الترجمة الخميرية
جمعية تطوير المجتمع الاسلامي الكمبودي
الترجمة النيبالية
جمعية أهل الحديث المركزية
الترجمة التايلاندية
مجموعة من جمعية خريجي الجامعات والمعاهد بتايلاند
الترجمة الصومالية
محمد أحمد عبدي
الترجمة الهوساوية
الترجمة الأمهرية
محمد صادق
الترجمة اليورباوية
أبو رحيمة ميكائيل أيكوييني
الترجمة الأورومية
الترجمة التركية للمختصر في تفسير القرآن الكريم
مركز تفسير للدراسات القرآنية
الترجمة الفرنسية للمختصر في تفسير القرآن الكريم
مركز تفسير للدراسات القرآنية
الترجمة الإندونيسية للمختصر في تفسير القرآن الكريم
مركز تفسير للدراسات القرآنية
الترجمة الفيتنامية للمختصر في تفسير القرآن الكريم
مركز تفسير للدراسات القرآنية
الترجمة البوسنية للمختصر في تفسير القرآن الكريم
مركز تفسير للدراسات القرآنية
الترجمة الإيطالية للمختصر في تفسير القرآن الكريم
مركز تفسير للدراسات القرآنية
الترجمة الفلبينية (تجالوج) للمختصر في تفسير القرآن الكريم
مركز تفسير للدراسات القرآنية
الترجمة الفارسية للمختصر في تفسير القرآن الكريم
مركز تفسير للدراسات القرآنية
Dr. Ghali - English translation
Muhsin Khan - English translation
Pickthall - English translation
Yusuf Ali - English translation
Azerbaijani - Azerbaijani translation
Sadiq and Sani - Amharic translation
Farsi - Persian translation
Finnish - Finnish translation
Muhammad Hamidullah - French translation
Korean - Korean translation
Maranao - Maranao translation
Abdul Hameed and Kunhi Mohammed - Malayalam translation
Salomo Keyzer - Flemish (Dutch) translation
Norwegian - Norwegian translation
Samir El - Portuguese translation
Polish - Polish translation
Romanian - Romanian translation
Elmir Kuliev - Russian translation
Albanian - Albanian translation
Tatar - Tatar translation
Japanese - Japanese translation
محمد جوناگڑھی - Urdu translation
Ma Jian - Chinese translation
Turkish - Turkish translation
King Fahad Quran Complex - Thai translation
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Abdullah Muhammad Basmeih - Malay translation
Hamza Roberto Piccardo - Italian translation
Indonesian - Indonesian translation
Bubenheim & Elyas - German / Deutsch translation
Bosnian - Bosnian translation
Hasan Efendi Nahi - Albanian translation
Sherif Ahmeti - Albanian translation
Sahih International - English translation
Czech - Czech translation
Abul Ala Maududi(With tafsir) - English translation
Tajik - Tajik translation
Alikhan Musayev - Azerbaijani translation
Muhammad Saleh - Uighur; Uyghur translation
Abdul Haleem - English translation
Mufti Taqi Usmani - English translation
Muhammad Karakunnu and Vanidas Elayavoor - Malayalam translation
Sheikh Isa Garcia - Spanish; Castilian translation
Divehi - Divehi; Dhivehi; Maldivian translation
Abubakar Mahmoud Gumi - Hausa translation
Mahmud Muhammad Abduh - Somali translation
Knut Bernström - Swedish translation
Jan Trust Foundation - Tamil translation
Mykhaylo Yakubovych - Ukrainian translation
Uzbek - Uzbek translation
Diyanet Isleri - Turkish translation
Ministry of Awqaf, Egypt - Russian translation
Abu Adel - Russian translation
Burhan Muhammad - Kurdish translation
Dr. Mustafa Khattab, The Clear Quran - English translation
Dr. Mustafa Khattab - English translation
الترجمة الإنجليزية - مركز رواد الترجمة
الترجمة الفرنسية - محمد حميد الله
الترجمة البوسنية - مركز رواد الترجمة
الترجمة الصربية - مركز رواد الترجمة - جار العمل عليها
الترجمة الألبانية - مركز رواد الترجمة - جار العمل عليها
الترجمة اليابانية - سعيد ساتو
الترجمة التاميلية - عمر شريف
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس
الترجمة اللوغندية - المؤسسة الإفريقية للتنمية
الترجمة الإنكو بامبارا - ديان محمد
الترجمة العبرية
الترجمة الإنجليزية للمختصر في تفسير القرآن الكريم
الترجمة الروسية للمختصر في تفسير القرآن الكريم
الترجمة البنغالية للمختصر في تفسير القرآن الكريم
الترجمة الصينية للمختصر في تفسير القرآن الكريم
الترجمة اليابانية للمختصر في تفسير القرآن الكريم
ترجمة معاني القرآن الكريم - عادل صلاحي
عادل صلاحي
ﰡ
آية رقم 1
Vinamtakasa Mwenyezi Mungu viumbe Vyake vyote vilivyoko mbinguni na ardhini. Na Yeye ni Mshindi juu ya viumbe Vyake, Mwingi wa hekima katika uendeshaji mambo yao.
آية رقم 2
Ni Yake mamlaka ya mbinguni na ardhini na vilivyomo ndani yake. Yeye Ndiye Mmiliki Mwenye kuendesha mambo ya viumbe Vyake, Anahuisha na kufisha, na Yeye juu ya kila kitu ni Muweza, hakuna kinachomshinda Akikitaka kifanyike, Anachokitaka kinakuwa, na Asichokitaka hakiwi.
آية رقم 3
Yeye Ndiye wa Mwanzo Ambaye hakukuwa na chochote kabla Yake, na Ndiye wa Mwisho Ambaye hakuna kitu chochote baada Yake, na Ndiye Aliyejitokeza Ambaye hakuna kitu chochote juu Yake, na Ndiye wa ndani Ambaye hakuna kitu chochote kilicho karibu kuliko Yeye, na hakuna chochote kinachofichamana Kwake ardhini wala mbinguni, na Yeye ni Mjuzi wa kila kitu.
آية رقم 4
Yeye Ndiye Aliyeumba mbingu na ardhi kisha Akawa juu ya 'Arsh Yake iliyo juu ya viumbe Vyake vyote kuwa Juu kunakonasibiana na utukufu Wake. Anavijua vinavyoingia ardhini, miongoni mwa mbegu, mvua na visivyokuwa hivyo, na vinavyotoka humo miongoni mwa mimea, nafaka na matunda, na vinavyoshuka kutoka mbinguni, miongoni mwa mvua na vinginevyo, na vinvyopanda huko, miongoni mwa Malaika na matendo ( ya awaja), na Yeye , kutakasika ni Kwake, Yuko pamoja na nyinyi kwa ujuzi Wake popote mnapokuwa. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kuyaona matendo yenu mnayoyafanya na Atawalipa kwayo.
آية رقم 5
Ni Yake mamlaka ya mbinguni na ardhini, na Kwake Mwenyezi Mungu ndiko mwisho wa mambo ya viumbe huko Akhera na Atawalipa wao kwa matendo yao.
آية رقم 6
Anazitia saa za usiku zilizopungua ndani ya mchana na hivyo basi mchana ukaongezeka, na Anazitia saa za mchana ndani ya usiku, na hivyo basi usiku ukaongezeka. Na Yeye , kutakasika ni Kwake, ni Mjuzi wa yaliyomo ndani ya vifua vya viumbe Vyake.
آية رقم 7
Muaminini Mwenyezi Mungu na Mtume Wake Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, na mtoe katika mali amabayo Mwenyezi Mungu Amewaruzuku na Akawafanya nyinyi ni wasimamizi wa mali hayo. Basi wale walioamini miongoni mwenu, enyi watu, na wakatoa mali yao watapata malipo makubwa.
آية رقم 8
Na mna udhuru gani ya nyinyi kutokaubali upweke wa Mwenyezi Mungu na kutofuata sheria Zake kivitendo na hali Mtume anawalingania juu ya hilo na Mwenyezi Mungu Ashachukua ahadi zenu juu ya hilo, iwapo nyinyi ni wenye kumuamini Mwenyezi Mungu Muumba wenu?
آية رقم 9
Yeye Ndiye Anayemteremshia mja Wake Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, aya za Qur’ani zilizopambanuliwa zilizo wazi, ili Awatoe nyinyi kwa hizo kwenye giza la ukafiri na kuwatia kwenye mwangaza wa Imani. Na hakika Mwenyezi Mungu, kwa kule kuwatoa nyinyi kwenye giza na kuwatia kwenye mwangaza, Anawarehemu rehema kunjufu katika maisha yenu ya sasa ya ulimwenguni na maisha yenu ya baadaye, na awalipe malipo mazuri kabisa.
آية رقم 10
Na ni kitu gani kinachowazuia nyinyi kutoa katika njia ya Mwenyezi Mungu? Hakika ni kwamba Mwenyezi Mungu Ndiye Mwenye urithi wa mbingu na ardhi, Anavirithi vyote vilivyomo humo, na hatasalia yoyote kuwa ni mwenye kumiliki chochote humo. Hawalingani kimalipo na thawabu wale waliotoa kabla ya ufunguzi wa Makkah na wakapigana na wakanushaji na wasiokuwa wao, kwani wao wana daraja kubwa zaidi mbele ya Mwenyezi Mungu kuliko wale waliotoa katika njia ya Mwenyezi Mungu baada ya ufunguzi na wakapigana na wakanushaji, na kila mojawapo ya makundi mawili haya Mwenyezi Mungu Ameliahidi Pepo. Na Mwenyezi Mungu ni Mtambuzi wa matendo yenu, hakuna chchote katika hayo kinachofichamana Kwake, na Atawalipa nyinyi kwa hayo.
آية رقم 11
Ni yupi yule anayetoa katika njia ya Mwenyezi Mungu kwa kutaka thawabu kutoka ndani ya moyo wake bila kusimanga wala kuudhi, ili Amuengezee Mola wake malipo na thawabu na apate malipo mema nayo ni Pepo?
آية رقم 12
Siku utakapowaona Waumini wa kiume na Waumini wa kike ikitembea nuru yao juu ya njia ya Ṣirāṭ mbele yao na upande wao wa kulia kwa kadiri ya matendo yao mema na waambiwe, «Bishara yenu leo ni kuingia kwenye mabustani ya Peponi yaliyo makunjufu ambayo chini ya miti yake inapita mito, hamtatolewa humo milele.» Malipo hayo ndiyo kufuzu kwenu kukubwa huko Akhera.
آية رقم 13
Siku watakaposema wanafiki wa kiume na wanafiki wa kike wakiwaambia Waumini, «Tungojeeni tupate mwangaza wa nuru yenu!» Hapo Malaika wawaambie, «Rudini nyuma yenu mtafute nuru (kwa njia ya kuwafanyia shere). Hapo watenganishwe baina yao kwa kuwekwa kizuizi cha ukuta wenye mlango ambao ndani yake , upande wa Waumini, mna rehema, na nje yake, upande wa wanafiki kuna adhabu.
آية رقم 14
Hapo wale wanafiki wawaite Waumini kwa kusema, «Kwani hatukuwa na nyinyi duniani tukitekeleza ibada za Dini kama nyinyi?» Na Waumini wawaambie, «Ndio, mlikuwa na sisi kidhahiri, lakini nyinyi mlijiangamiza wenyewe kwa unafiki na kufanya maasia, na mkingojea kwa hamu Nabii afe na Waumini wapatikane na mikasa, mkakufanyia shaka kule kufufuliwa baada ya kufa, na yakawadanganya nyinyi matumaini yenu ya urongo na mkasalia katika hali hiyo mpaka mauti yakawajia. Na Shetani aliwadanganya nyinyi kuhusu Mwenyezi Mungu.
آية رقم 15
Leo haitakubaliwa badala kutoka kwa yoyote miongoni mwenu, enyi wanafiki, ili ajifidie kwayo na adhabu ya Mwenyezi Mungu wala kutoka kwa wale waliomkanusha Mwenyezi Mungu na Mtume Wake. mwisho wenu nyote ni Moto, huo ni makao mnayostahili zaidi kuliko makao yoyote, na mwisho mbaya kabisa ni huo.
آية رقم 16
Je haujafika wakati kwa wale waliomuamini Mwenyezi Mungu na Mtume wake na wakafuata uongofu Wake kulainika nyoyo zao anapotajwa Mwenyezi Mungu na kuisikia Qur’ani, na wasiwe ni wenye ugumu wa nyoyo kama walivyokuwa wale waliopewa Vitabu kabla yao, kati ya Mayahudi na Wanaswara, ambao walipitiwa na muda mrefu wakayageuza maneno ya Mwenyezi Mungu na nyoyo zao zikawa ngumu, na wengi miongoni mwao wakatoka nje ya utiifu wa Mwenyezi Mungu? Katika aya hii pana kuhimiza ulainifu na unyenyekevu kwa Mwenyezi Mungu, Aliyetakasika, wakati wa kuyasikia yale Aliyoyateremsha Mwenyezi Mungu ya Kitabu na Hekima, na kujihadhari na kujifananisha na Mayahudi na Wanaswara katika ususuwavu wa nyoyo zao na kutoka nje ya utiifu wa Mwenyezi Mungu.
آية رقم 17
Jueni kwamba Mwenyezi mungu, Aliyetakasika na kutukuka, Anaihuisha ardhi kwa mvua baada ya kufa kwake ikatoa mimea. Basi vilevile Mwenyezi Mungu ni Muweza wa kuhuisha wafu Siku ya Kiyama, na Ndiye Muweza wa kuzilainisha nyoyo baada ya kususuwaa kwake. Kwa hakika tumewafunulia wazi dalili za uweza wetu, huenda nyinyi mkazielewa na kwa hivyo mkawaidhika.
آية رقم 18
Hakika ya wale wanaume na wanawake wanaotoa sadaka kutokana na mali yao na wakatumia katika njia ya Mwenyezi Mungu matumizi zikiwa radhi nyoyo zao, kwa kutafuata radhi za Mwenyezi Mungu Aliyetukuka, wataongezewa malipo mema ya hayo, na juu ya hayo watapata malipo mengi, nayo ni Pepo.
آية رقم 19
Na wale waliomuamini Mwenyezi Mungu na Mitume Wake na wasimbague yoyote miongoni mwao, hao ndio wakweli iliyokamilika imani yao kwa kile walichokuja nacho Mitume, kiitikadi, kimaneno na kivitendo, na ndio mashahidi mbele ya Mola wao; watapata malipo yao mengi kutoka kwa Mwenyezi Mungu na nuru yao kubwa Siku ya Kiyama. Na wale waliokufuru na kukanusha dalili zetu na hoja zetu, wao ndio watu wa Motoni, hawatakuwa na malipo mema wala nuru.
آية رقم 20
Jueni, enyi watu, kwamba uhai wa kilimwengu ni mchezo na pumbao ya miili kuchezea na nyoyo kupumbaa, na pambo la nyinyi kujipamba nalo, na kuoneshana baina yenu kwa vitu vyake vya starehe, na kushindana kwa wingi wa mali na watoto. Mfano wake ni kama ule wa mvua ambayo mimea yake iliwafurahisha wakulima, kisha ikasinyaa na kukauka, ukaiona imekuwa rangi ya manjano baada ya kuwa rangi ya kijani, kisha ikawa ni yenye kukatikakatika na kuwa mikavu na kusagikasagika. Na huko Akhera kuna adhabu kali kwa makafiri na msamaha wa Mwenyezi Mungu na radhi Zake kwa watu wenye kuamini. Na haukuwa uhai wa kilimwengu, kwa mwenye kuushughulikia hali ya kusahau Akhera yake, isipokuwa ni starehe yenye udanganyifu.
آية رقم 21
Shindaneni, enyi watu, katika kukimbilia sababu za kusamehewa kwa kutubia kidhati na kujiepusha na maasia, ili mlipwe msamaha kutoka kwa Mola wenu na Pepo ambayo upana wake ni kama upana wa mbingu na ardhi, nayo imetayarishiwa wale waliompwekesha Mwenyezi mungu na wakawafuata Mitume Wake. Hizo ni nyongeza za Mwenyezi Mungun Anazompa Anayemtaka miongoni mwa viumbe Vyake. Pepo haipatikani isipokuwa kwa rehema ya mwenyezi Mungu na nyongeza Zake na matendo mema. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye nyongeza kubwa kwa waja Wake Waumini.
آية رقم 22
Hampatikani na msiba wowote, enyi watu, kwenye ardhi wala ndani ya nafsi zenu, utokanao na magonjwa, njaa na ndwele, isipokuwa umeandikwa kwenye Ubao Uliyohifadhiwa kabla ya kuumbwa viumbe. Hakika hilo, kwa Mwenyezi Mungu, ni jambo sahali.
آية رقم 23
Ili msisikitike kwa mlichokikosa cha ulimwengu na msifurahike furaha ya kiburi na majivuno. Na mwenyezi mungu Hampendi kila mwenye kujiona kwa alichopewa cha ulimwengu, mwenye kujifahiri nacho juu ya wengine.
آية رقم 24
Hawa wenye kujiona ndio wale wanaoyafanyia ubahili mali yao, wasiyatoe katika njia ya Mwenyezi Mungu, na wakawaamuru watu wawe mabahili kwa kuwapambia huo ubahili. Na yoyote anayezunguka nyuma kwa kuacha kumtii Mwenyezi mungu hamdhuru yoyote isipokuwa nafsi yake, na hatamdhuru Mwenyezi Mungu chochote, kwani Mwenyezi Mungu Ndiye Mkwasi Asiyehitajia viumbe vyake, Mwenye kuhimidiwa Ambaye Ana kila sifa njema iliyokamilika na kila tendo zuri ambalo Anastahiki kushukuriwa kwalo.
آية رقم 25
Hakika tumetumiliza Mitume wetu kwa hoja zilizo wazi na kuwateremshia Vitabu vyenye hukumu na sheria, na tukateremsha mizani ili watu waamiliane baina yao kwa uadilifu, na tukateremsha chuma chenye nguvu nyingi na manufaa mengi kwa watu, na ili Mwenyezi Mungu Amjue, ujuzi wenye kujitokeza kwa watu, yule anayetetea Dini Yake na Mitume Wake kwa ghaibu. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye nguvu Asiyetendeshwa nguvu, ni Mshindi hakuna anayeweza kushindana na Yeye.
آية رقم 26
Na hakika tuliwatumiliza Nūḥ na Ibrāhīm kwa watu wao, na tukajaalia kwenye kizazi chao unabii na vitabu vilivyoteremshwa. Basi miongoni mwa watu wa kizazi chao kuna walioongoka kwenye haki, na wengi kati yao wametoka nje ya utiifu wa Mwenyezi Mungu.
آية رقم 27
Kisha tukafuatisha, kwenye athari za Nūḥ na Ibrāhīm, Mitume wetu tiliowatumiliza kwa hoja zilizo wazi, na tukamfuatisha 'Īsā mwana wa Maryam na tukampa Injili, na tukajaalia ndani ya nyoyo za wale waliomfuata na kuwa kwenye dini yake ulaini na huruma, wakawa wanapendana wao kwa wao, na walizusha taratibu za kuabudu, kwa kupitisha kiasi katika ibada, ambazo hatukuwalazimisha nazo isipokuwa ni wao wenyewe waliojilazimisha nazo kwa lengo la kupata radhi za Mwenyezi Mungu, lakini hawakusimama nazo vile inavyotakiwa kusimama. Basi tukawapa wale walioamini miongoni mwao malipo yao kulingana na Imani yao, na wengi miongoni mwao ni wenye kutoka nje ya utiifu wa Mwenyezi Mungu na ni wenye kumkanusha Nabii Wake Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie.
آية رقم 28
Enyi mlioamini! Fuateni amri za Mwenyezi Mungu na mjiepushe na makatazo Yake na muaminini Mtume Wake, Atawapa rehema Zake mara mbili zaidi, na Atawafanya muwe na nuru ambayo kwayo mnajiongoza na Atawasamehe dhambi zenu. Na Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa msamaha kwa waja Wake, ni Mwenye kuwarehemu.
آية رقم 29
Mwenyezi Mungu Aliyetukuka Amewapa haya yote ili wapate kujua watu waliopewa Vitabu ambao hawakumuamini Mtume Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, kwamba wao hawawezi chochote kujipa wao wenyewe nyongeza za kheri za Mwenyezi Mungu wala kuwapatia wengine, na kwamba nyongeza zote ziko kwa Mwenyezi Mungu. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye wema mkubwa na vipewa vingi kwa viumbe Vyake.
تقدم القراءة