ترجمة معاني سورة المدّثر باللغة السواحلية من كتاب الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس
ﰡ
آية رقم 1
ﮪﮫ
ﮬ
Ewe uliojifinika nguo zako!
آية رقم 2
ﮭﮮ
ﮯ
Inuka kutoka kwenye malazi yako owaonye watu adhabu ya Menyezi Mungu.
آية رقم 3
ﮰﮱ
ﯓ
Na umkusudie Mola wako, Peke Yake, kwa kumtukuza, kumpwekesha na kumuabudu.
آية رقم 4
ﯔﯕ
ﯖ
Na usafishe nguo zako kutokana na najisi, kwani usafi wa nje ni katika kutimia usafi wa ndani.
آية رقم 5
ﯗﯘ
ﯙ
Na uendelee daima kuyaepuka masanamu na mizimu, na matendo ya ushirikina yote usiyakaribie.
آية رقم 6
ﯚﯛﯜ
ﯝ
Na usitoe kitu kumpa mtu kwa lengo la kupata zaidi ya hiko. Na kwa ajili ya kupata radhi ya Mwenyezi Mungu,
آية رقم 7
ﯞﯟ
ﯠ
vumilia juu ya maamrisho na makatazo.
آية رقم 8
ﯡﯢﯣﯤ
ﯥ
Pindi patakapopulizwa kwenye barugumu mpulizo wa Ufufuzi na Uenezaji,
آية رقم 9
ﯦﯧﯨﯩ
ﯪ
wakati huo ni wakati ambao ni mgumu kwa makafiri;
آية رقم 10
ﯫﯬﯭﯮ
ﯯ
si rahisi kwao kusalimika na yale walionayo ya kujadiliwa hesabu zao na vituko vingine vikubwa.
آية رقم 11
ﯰﯱﯲﯳ
ﯴ
Niache mimi, ewe Mtume, na huyu niliyemuumba ndani ya tumbo la mamake akiwa peke yake, hana mali wala watoto.
آية رقم 12
ﯵﯶﯷﯸ
ﯹ
Nikamfanya awe na mali mengi yenye kuenea na watoto waliyoko na yeye hapo Makkah hawamuondokei. Na
آية رقم 13
ﯺﯻ
ﯼ
nikamsahilishia kwa kumrahisishia njia za maisha. Kisha yeye anatarajia, baada ya vitu hivi alivyopewa,
آية رقم 14
ﯽﯾﯿ
ﰀ
nimuongezee kwenye mali yake na watoto wake na huku yeye amenikanusha. Mambo sivyo kama anavyodai huyu mwenye kuasi, mtenda dhambi.
آية رقم 15
ﰁﰂﰃﰄ
ﰅ
Simuongezei zaidi ya hiko nilichompa,
آية رقم 16
ﰆﰇﰈﰉﰊﰋ
ﰌ
kwa kuwa yeye alikuwa mshindani mkanushaji wa Qur’ani na hoja za Mwenyezi Mungu kwa viumbe Wake.
آية رقم 17
ﰍﰎ
ﰏ
Nitambebesha mateso magumu na usumbufu usio na mapumziko. Anayekusudiwa hapa ni Al-Walid mwana wa Al-Mughi rah aliyekuwa akishindana na haki na akijitokeza kupigana vita na Mwenyezi Mungu na Mtume Wake. Haya ndiyo malipo ya kila mwenye kushindana na haki na kuipiga vita.
آية رقم 18
ﰐﰑﰒ
ﰓ
Kwa kweli yeye aliwaza ndani ya nafsi yake akatayarisha la kusema kumtukana Mtume, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, na Qur’ani.
آية رقم 19
ﭑﭒﭓ
ﭔ
Hivyo basi akalaaniwa na akastahili, kwa hilo, maangamivu: alijiandaa vipi ndani ya nafsi yake kwa hayo matukano?
آية رقم 20
ﭕﭖﭗﭘ
ﭙ
Kisha pia akalaaniwa.
آية رقم 21
ﭚﭛ
ﭜ
Kisha yeye alifikiria kuhusu kile alichokipanga na kukitayarisha cha kuitia dosari Qur’ani.
آية رقم 22
ﭝﭞﭟ
ﭠ
Kisha akafinya uso wake na akazidi katika hali ile ya ukunjaji uso kwa kukosa hila za kufanya na kutopata ila yoyote ya kuitia dosari Qur’ani.
آية رقم 23
ﭡﭢﭣ
ﭤ
Kisha akarudi kuipa mgongo haki na akajiona ni mkubwa wa kutofaa kuikubali,
آية رقم 24
ﭥﭦﭧﭨﭩﭪ
ﭫ
hapo akasema kuhusu Qur’ani, «Haya anayoyasema Muhammad si chochote isipokuwa ni uchawi uliopokewa kutoka kwa watu wa mwanzo waliopita.
آية رقم 25
ﭬﭭﭮﭯﭰ
ﭱ
Haikuwa hi Qur’ani isipokuwa ni maneno ya viumbe ambayo Muhammad amejifunza kutoka kwao kisha akadai kuwa yanatoka kwa Mwenyezi Mungu.»
آية رقم 26
ﭲﭳ
ﭴ
Basi nitamuingiza kwenye moto wa Jahanamu ili alionje joto lake na achomeke kwa moto wake.
آية رقم 27
ﭵﭶﭷﭸ
ﭹ
Na ni lipi lililokujulisha wewe ni kitu gani hiyo Jahanamu?
آية رقم 28
ﭺﭻﭼﭽ
ﭾ
Haibakishi nyama wala haiachi mfupa isipokuwa huvichoma.
آية رقم 29
ﭿﮀ
ﮁ
Unageuza ngozi ya mwili, unazifanya ngozi kuwa nyeusi na unazichoma.
آية رقم 30
ﮂﮃﮄ
ﮅ
Wanasimamia mambo yake na kushikilia kazi ya kuwatesa watu wake Malaika kumi na tisa katika washika zamu wa Motoni wenye nguvu.
Na hatukuwafanya washika hazina wa Motoni isipokuwa miongoni mwa Malaika washupavu. Na hatukuiweka idadi hiyo isipokuwa kuwatahini wale waliomkufuru Mwenyezi Mungu, na ili imani ya yakini ipatikane kwa wale Mayahudi na Wanaswara waliopewa Vitabu kwamba yaliyokuja ndani ya Qur’ani juu ya washika hazina wa Motoni ni ukweli utokao kwa Mwenyezi Mungu Aliyetukuka, kwani hayo yanaafikiana na vitabu vyao, na ili Waumini wazidi kumuamini Mwenyezi Mungu na Mtume Wake na waifuate Sheria Yake kivitendo, na ili wasilifanyie shaka hilo wale Mayahudi na Wanaswara waliopewa Vitabu wala wale wenye kumuamini Mwenyezi Mungu na Mtume Wake, na ili wapate kusema wale wenye unafiki ndani ya nyoyo zao na makafiri, «Ni lipi alilolikusudia Mwenyezi Mungu kwa idadi hii ya ajabu?» Kwa mfano wa hayo yaliyotajwa, Mwenyezi Mungu Anampoteza Anayetaka kumpoteza na Anamuongoza Anayetaka kumuongoza. Na hakuna ajuwaye idadi ya askari wa Mola wako, na miongoni mwao ni Malaika, isipokuwa Mwenyezi Mungu Peke Yake. Na haukuwa huu Moto isipokuwa ni ukumbusho na mazingatio kwa watu.
آية رقم 32
ﯥﯦ
ﯧ
Mambo sivyo kama walivyotaja ya ukanushaji Mtume katika yale aliyokuja nayo! Anaapa Mwenyezi Mungu, Aliyetakasika na kila sifa ya upungufu, kwa mwezi,
آية رقم 33
ﯨﯩﯪ
ﯫ
na kwa usiku unapogeuka kwenda zake,
آية رقم 34
ﯬﯭﯮ
ﯯ
na kwa asubuhi inapotoa mwangaza na kufunuka,
آية رقم 35
ﯰﯱﯲ
ﯳ
hakika Moto ni mojawapo ya mambo makubwa,
آية رقم 36
ﯴﯵ
ﯶ
kwa ajili ya kuwaonya na kuwatisha watu,
آية رقم 37
kwa anayetaka miongoni mwenu kujiweka karibu na Mola wake kwa kufanya matendo ya utiifu, au kujikalisha nyuma kwa kufanya matendo ya uasi.
آية رقم 38
ﯿﰀﰁﰂﰃ
ﰄ
Kila nafsi imefungwa na kuwekwa rahani kwa ilichokitenda, miongoni mwa matendo mema au mabaya, kwa kukichuma. Haifunguliwi mpaka itekeleze haki zilizo juu ya lazima yake na ipatiwe mateso yanayostahili kupatiwa.
آية رقم 39
ﰅﰆﰇ
ﰈ
Isipokuwa Waislamu waliotakaswa, watu wa upande wa kulia waliojikomboa shingo zao kwa utiifu.
آية رقم 40
ﰉﰊﰋ
ﰌ
Wao watakuwa kwenye mabustani ya Peponi ambayo sifa zake hazifikiwi ukomo. Watakuwa wakiulizana wao kwa wao
آية رقم 41
ﰍﰎ
ﰏ
kuhusu makafiri waliojikosea nafsi zao,
آية رقم 42
ﰐﰑﰒﰓ
ﰔ
«Ni lipi lililowaingiza kwenye moto wa Jahanamu na likawafanya
آية رقم 43
ﰕﰖﰗﰘﰙ
ﰚ
mlionje joto lake lililo kali sana?» Wahalifu waseme , «Hatukuwa ni miongoni mwa wanaoswali duniani,
آية رقم 44
ﰛﰜﰝﰞ
ﰟ
na hatukuwa tukitoa sadaka na kuwafanyia wema wahitaji na maskini,
آية رقم 45
ﰠﰡﰢﰣ
ﰤ
na tulikuwa tukizungumza maneno ya ubatilifu na watu wa upotofu na upotevu,
آية رقم 46
ﰥﰦﰧﰨ
ﰩ
na tulikuwa tukiikanusha Siku ya kuhesabiwa na kulipwa,
آية رقم 47
ﰪﰫﰬ
ﰭ
mpaka kifo kikatujia na hali sisi tuko kwenye mambo hayo mabaya ya upotevu.
آية رقم 48
ﭑﭒﭓﭔ
ﭕ
Basi hayatawafalia neno maombezi ya wenye kuombea wote, miongoni mwa Malaika, Manabii na wengineo, kwa kuwa aombewaye ni yule aliyechaguliwa na Mwenyezi Mungu na akamuidhinisha mwenye kumuombea.
آية رقم 49
ﭖﭗﭘﭙﭚ
ﭛ
Basi wana nini hawa washirikina wamejiepusha na Qur’ani na
آية رقم 50
ﭜﭝﭞ
ﭟ
mawaidha yaliyomo ndani yake? Kama kwamba wao ni pundamilia wanaobabaika
آية رقم 51
ﭠﭡﭢ
ﭣ
wanaomkimbia simba mshambulizi.
آية رقم 52
Lakini kila mmoja, miongoni mwa hawa washirikina, ana matumaini ateremshiwe kitabu kutoka mbinguni kilichokunjuliwa kama kile kilichoteremshiwa Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie.
آية رقم 53
ﭮﭯﭰﭱﭲﭳ
ﭴ
Mambo si hivyo kama wanavyodai. Ukweli ni kwamba wao hawaiogopi Akhera wala hawaamini kuwa kuna kufufuliwa na kulipwa.
آية رقم 54
ﭵﭶﭷ
ﭸ
Ni kweli kwamba Qur’ani ni mawaidha yenye ufasaha, yanayotosha kuwafanya wao wawaidhike.
آية رقم 55
ﭹﭺﭻ
ﭼ
Anayetaka kuwaidhika, basi na awaidhike kwa yaliyomo ndani yake na anufaike na uongofu wake.
آية رقم 56
Na hawawaidhiki kwayo isipokuwa iwapo Mwenyezi Mungu Amewatakia kuongoka. Yeye, kutakasika na sifa za upungufu ni Kwake, Ndiye Anayestahiki kuogopewa na kutiiwa, na Ndiye Anayestahiki kumsamehe anayemuamini Yeye na kumtii.
تقدم القراءة