ترجمة معاني سورة الإنفطار باللغة السواحلية من كتاب الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس
ﰡ
آية رقم 1
ﭑﭒﭓ
ﭔ
Pindi mbingu zitakapopasuka na ukaharibika mpango wake.
آية رقم 2
ﭕﭖﭗ
ﭘ
Na pindi nyota zitakapoangukiana.
آية رقم 3
ﭙﭚﭛ
ﭜ
Na pindi Mwenyezi Mungu Atakapozifanya bahari kulipuka na maji yake kutoweka.
آية رقم 4
ﭝﭞﭟ
ﭠ
Na pindi makaburi yatakapogeuzwa kwa kufufuliwa waliokuwamo ndani yake.
آية رقم 5
ﭡﭢﭣﭤﭥ
ﭦ
Wakati huo itajua kila nafsi vitendo vyake vyote ilivyovifanya, vilivyotangulia na vilivyoahirika na italipwa kwa vitendo hivyo.
آية رقم 6
ﭧﭨﭩﭪﭫﭬ
ﭭ
Ewe binadamu unayekanusha kufufuliwa! Ni kipi kilichokufanya uhadaike na ughurike kuhusu Mola wako Mpaji Mwenye kheri nyingi, Anayestahiki kushukuriwa na kutiiwa?
آية رقم 7
ﭮﭯﭰﭱ
ﭲ
Kwani si Yeye Aliyekuumba, Akalisawazisha umbo lako, Akakuweka katika hali ya sawa na Akakurekibisha ili uweze kutekeleza nyadhifa zako,
آية رقم 8
ﭳﭴﭵﭶﭷﭸ
ﭹ
katika sura yoyote ile Aliyoitaka Akakuumba?
آية رقم 9
ﭺﭻﭼﭽ
ﭾ
Mambo hayako kama vile mnavyosema kwamba nyinyi mna haki ya kumuabudu asiyekuwa Mwenyezi Mungu. Bali nyinyi mnaikanusha Siku ya Hesabu na Malipo.
آية رقم 10
ﭿﮀﮁ
ﮂ
Na mjue kuwa wako na nyinyi Malaika wachunguzi,
آية رقم 11
ﮃﮄ
ﮅ
watukufu kwa Mwenyezi Mungu, waandishi wa yale waliyowakilishwa kuyadhibiti. Hakiwapiti, katika vitendo vyenu na siri zenu, chochote.
آية رقم 12
ﮆﮇﮈ
ﮉ
Wanayajua mnayoyafanya, ya kheri au ya shari.
آية رقم 13
ﮊﮋﮌﮍ
ﮎ
Hakika wachamungu wanaotekeleza haki za Mwenyezi Mungu na haki za waja wake watakuwa kwenye neema.
آية رقم 14
ﮏﮐﮑﮒ
ﮓ
Hakika watu waovu waliopuuza haki za Mwenyezi Mungu na haki za waja wake watakuwa katika Moto mkali.
آية رقم 15
ﮔﮕﮖ
ﮗ
Ukali wake, Moto huo, utawapata Siku ya Malipo.Na wala wao hawatakuwa ni wenye kughibu,
آية رقم 16
ﮘﮙﮚﮛ
ﮜ
wakawa hawamo ndani ya Moto wa Jahanamu, si kwa kutoka wala kwa kufa.
آية رقم 17
ﮝﮞﮟﮠﮡ
ﮢ
Ni kipi kinachokujuza ni upi utukufu wa Siku ya Hesabu?
آية رقم 18
ﮣﮤﮥﮦﮧﮨ
ﮩ
Kisha ni kipi kinachokujuza ni upi utukufu wa Siku ya Hesabu?
آية رقم 19
Siku ya Hesabu, hataweza yoyote kumnufaisha yoyote. Na amri zote Siku Hiyo ni za Mwenyezi Mungu Peke yake Ambaye hakuna mwenye kumshinda, wala hakuna mwenye kumtendesha nguvu, wala hakuna mwenye kushindana na Yeye.
تقدم القراءة