ترجمة معاني سورة الطارق باللغة السواحلية من كتاب الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس
ﰡ
آية رقم 1
ﭑﭒ
ﭓ
Mwenyezi Mungu Anaapa kwa mbingu na nyota yenye kuchomoza usiku.
آية رقم 2
ﭔﭕﭖﭗ
ﭘ
Na ni lipi lilokujulisha ni ukubwa gani wa nyota hiyo?
آية رقم 3
ﭙﭚ
ﭛ
Hiyo ni nyota ing’arao na kuzagaa.
آية رقم 4
ﭜﭝﭞﭟﭠﭡ
ﭢ
Hakuna nafsi yoyote isipokuwa amewakilishwa kwayo Malaika mwenye kuchunguza na kusjili amali zake ili ihesabiwe Siku ya Kiyama.
آية رقم 5
ﭣﭤﭥﭦ
ﭧ
Basi aangalie binadamu mwenye kukanusha kufufuliwa ameumbwa kwa kitu gani? Ili ajue kuwa kurudisha umbo lake mara ya pili si vigumu kama kuumbwa mara ya kwanza.
آية رقم 6
ﭨﭩﭪﭫ
ﭬ
Aliumbwa kwa manii yenye kupenyeza ndani ya uzao kwa haraka.
آية رقم 7
ﭭﭮﭯﭰﭱ
ﭲ
Yatokayo kwenye mgongo wa mwnamume na kifua cha mwanamke.
آية رقم 8
ﭳﭴﭵﭶ
ﭷ
Hakika yule Aliyemuumba binadamu kwa maji haya ni muweza wa kumrudisha kwenye uhai baada ya kufa.
آية رقم 9
ﭸﭹﭺ
ﭻ
Siku zitakapofunuliwa wazi siri ziliofichwa na nafsi na kupambanuliwa njema na mbovu.
آية رقم 10
ﭼﭽﭾﭿﮀﮁ
ﮂ
Binadamu hatakuwa na nguvu ya kuitetea nafsi yake wala hatakuwa na mtetezi wa kumwepushia adhabu ya Mwenyezi Mungu.
آية رقم 11
ﮃﮄﮅ
ﮆ
Na Anaapa kwa mbingu yenye mvua ya kukaririka.
آية رقم 12
ﮇﮈﮉ
ﮊ
Na ardhi yenye pasuko za kufanya mimea ichipuke.
آية رقم 13
ﮋﮌﮍ
ﮎ
Hakika Qur’ani ni neno lenye kupambanua baina ya haki na batili.
آية رقم 14
ﮏﮐﮑ
ﮒ
Na si upuuzi. Haifai kiumbe kuapa kwa asiyekuwa Mwenyezi Mungu. Akifanya hivyo atakuwa amemshirikisha Mwenyezi Mungu.
آية رقم 15
ﮓﮔﮕ
ﮖ
Hakika wenye kumkanusha Mtume, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, na Qur’ani wanafanya vitimbi na mipango ili kuipinga haki na kuitilia nguvu batili.
آية رقم 16
ﮗﮘ
ﮙ
Na Mimi nafanya vitimbi kuidhihirisha haki ingawa makafiri wanatukia.Usiwe na haraka nao, ewe Mtume, kutaka wateremshiwe adhabu.
آية رقم 17
ﮚﮛﮜﮝ
ﮞ
Wape muhula uwangojee muda mchache wala usiwafanyie haraka, utaona adhabu itakayowafikia, mateso na maangamivu.
تقدم القراءة