ترجمة معاني سورة الطارق باللغة السواحلية من كتاب الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس

الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس

آية رقم 1
Mwenyezi Mungu Anaapa kwa mbingu na nyota yenye kuchomoza usiku.
آية رقم 2
Na ni lipi lilokujulisha ni ukubwa gani wa nyota hiyo?
آية رقم 3
Hiyo ni nyota ing’arao na kuzagaa.
آية رقم 4
Hakuna nafsi yoyote isipokuwa amewakilishwa kwayo Malaika mwenye kuchunguza na kusjili amali zake ili ihesabiwe Siku ya Kiyama.
آية رقم 5
Basi aangalie binadamu mwenye kukanusha kufufuliwa ameumbwa kwa kitu gani? Ili ajue kuwa kurudisha umbo lake mara ya pili si vigumu kama kuumbwa mara ya kwanza.
آية رقم 6
Aliumbwa kwa manii yenye kupenyeza ndani ya uzao kwa haraka.
آية رقم 8
Hakika yule Aliyemuumba binadamu kwa maji haya ni muweza wa kumrudisha kwenye uhai baada ya kufa.
آية رقم 9
Siku zitakapofunuliwa wazi siri ziliofichwa na nafsi na kupambanuliwa njema na mbovu.
آية رقم 10
Binadamu hatakuwa na nguvu ya kuitetea nafsi yake wala hatakuwa na mtetezi wa kumwepushia adhabu ya Mwenyezi Mungu.
آية رقم 11
Na Anaapa kwa mbingu yenye mvua ya kukaririka.
آية رقم 12
Na ardhi yenye pasuko za kufanya mimea ichipuke.
آية رقم 13
Hakika Qur’ani ni neno lenye kupambanua baina ya haki na batili.
آية رقم 14
Na si upuuzi. Haifai kiumbe kuapa kwa asiyekuwa Mwenyezi Mungu. Akifanya hivyo atakuwa amemshirikisha Mwenyezi Mungu.
آية رقم 15
Hakika wenye kumkanusha Mtume, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, na Qur’ani wanafanya vitimbi na mipango ili kuipinga haki na kuitilia nguvu batili.
آية رقم 16
Na Mimi nafanya vitimbi kuidhihirisha haki ingawa makafiri wanatukia.Usiwe na haraka nao, ewe Mtume, kutaka wateremshiwe adhabu.
آية رقم 17
Wape muhula uwangojee muda mchache wala usiwafanyie haraka, utaona adhabu itakayowafikia, mateso na maangamivu.
تقدم القراءة