ترجمة معاني سورة البروج باللغة السواحلية من كتاب الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس
ﰡ
آية رقم 1
ﭛﭜﭝ
ﭞ
Mwenyezi Mungu Anaapa kwa mbingu zenye njia za kupitia jua na mwezi.
آية رقم 2
ﭟﭠ
ﭡ
Na kwa Siku ya Kiyama ambayo Amewaahidi viumbe kuwa Atawakusanya.
آية رقم 3
ﭢﭣ
ﭤ
Na kwa shahidi, mwenye kutoa ushahidi, na mwenye kutolewa ushahidi juu yake. Mwenyezi Mungu Huapa kwa Anachokitaka. Lakini kiumbe hafai kuapa kwa asiyekuwa Mwenyezi Mungu. Kuapa kwa asiyekuwa Mwenyezi Mungu ni ushirikina.
آية رقم 4
ﭥﭦﭧ
ﭨ
Wamelaaniwa waliofukua chini ya ardhi shimo kubwa ili kuwatesa Waumini.
آية رقم 5
ﭩﭪﭫ
ﭬ
Wakawasha moto mkubwa wenye kuni nyingi.
آية رقم 6
ﭭﭮﭯﭰ
ﭱ
Wakawa wamekaa kwenye kingo za shimo hilo.
آية رقم 7
ﭲﭳﭴﭵﭶﭷ
ﭸ
Wakishuhudia vitendo vya mateso na adhabu wanavyowafanyia Waumini.
آية رقم 8
Na hawakuwatesa mateso hayo isipokuwa wenye kuteswa walikuwa wanamuamini Mwenyezi Mungu Mshindi Asiyeshindwa, Mhimidiwa wa maneno Yake vitendo Vyake na sifa Zake.
آية رقم 9
Mwenye ufalme wa mbingu na ardhi Ambaye, kutakasika na sifa za upungufu ni kwake, Anashuhudia kila kitu, hakuna kinachofichika kwake.
آية رقم 10
Hakika, wale waliowachoma kwa moto Waumini, wa kike na wa kiume, ili kuwazuia watu na dini ya Mwenyezi Mungu, kisha wasitubie, watapata, Siku ya Akhera, adhabu ya Jahanamu na watapata adhabu kali yenye kuchoma.
آية رقم 11
Wale waliomuamini Mwenyezi Mungu na Mtume Wake na wakafanya amali njema, watapata Pepo ambayo chini ya majumba yake ya kifahari yapita mito. Huko ni kufaulu kukubwa.
آية رقم 12
ﮮﮯﮰﮱ
ﯓ
Hakika malipizo ya Mola wako kwa maadui Zake na mateso Yake juu yao ni mazito.
آية رقم 13
ﯔﯕﯖﯗ
ﯘ
Ndiye Yeye Mwenye kuanzisha kuumba na kisha kurudisha.
آية رقم 14
ﯙﯚﯛ
ﯜ
Ndiye Yeye Mwingi wa kusamehe kwa wenye kutubia, Mwingi wa mapenzi kwa wanaoikurubisha kwake.
آية رقم 15
ﯝﯞﯟ
ﯠ
Mwenye Arshi tukufu.
آية رقم 16
ﯡﯢﯣ
ﯤ
Mfanya Alitakalo: hakuna kitu Anachotaka kiwe kisiwe.
آية رقم 17
ﯥﯦﯧﯨ
ﯩ
Je, ewe Mtume, imekufikia habari ya makundi yaliyokufuru na kukanusha Mitume walioletwa, ya
آية رقم 18
ﯪﯫ
ﯬ
Firauni na Thamūd, misiba na adhabu iliyowashukia? Hawakuzingatia kwa habari hiyo.
آية رقم 19
ﯭﯮﯯﯰﯱ
ﯲ
Bali waliokufuru waendelea kukanusha kwao, kama walivyokuwa waliokuja kabla yao.
آية رقم 20
ﯳﯴﯵﯶ
ﯷ
Na Mwenyezi Mungu Amewazunguka kwa Ujuzi na Uweza Wake, hakuna chenye kufichika Kwake kuhusu wao na vitendo vyao. Hii Qu’ani siyo kama wanavyodai wenye kukanusha katika washirikina kuwa ni mashairi na uchawi ndipo wakaikanusha.
آية رقم 21
ﯸﯹﯺﯻ
ﯼ
Bali hii ni Qur’ani kubwa iliyo tukufu,
آية رقم 22
ﯽﯾﯿ
ﰀ
iliyomo kwenye Ubao Uliohifadhiwa, haufikiwi na kubadilishwa wala kupotoshwa.
تقدم القراءة