ترجمة معاني سورة البروج باللغة السواحلية من كتاب الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس

الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس

آية رقم 1
Mwenyezi Mungu Anaapa kwa mbingu zenye njia za kupitia jua na mwezi.
آية رقم 2
Na kwa Siku ya Kiyama ambayo Amewaahidi viumbe kuwa Atawakusanya.
آية رقم 3
Na kwa shahidi, mwenye kutoa ushahidi, na mwenye kutolewa ushahidi juu yake. Mwenyezi Mungu Huapa kwa Anachokitaka. Lakini kiumbe hafai kuapa kwa asiyekuwa Mwenyezi Mungu. Kuapa kwa asiyekuwa Mwenyezi Mungu ni ushirikina.
آية رقم 4
Wamelaaniwa waliofukua chini ya ardhi shimo kubwa ili kuwatesa Waumini.
آية رقم 5
Wakawasha moto mkubwa wenye kuni nyingi.
Na hawakuwatesa mateso hayo isipokuwa wenye kuteswa walikuwa wanamuamini Mwenyezi Mungu Mshindi Asiyeshindwa, Mhimidiwa wa maneno Yake vitendo Vyake na sifa Zake.
Hakika, wale waliowachoma kwa moto Waumini, wa kike na wa kiume, ili kuwazuia watu na dini ya Mwenyezi Mungu, kisha wasitubie, watapata, Siku ya Akhera, adhabu ya Jahanamu na watapata adhabu kali yenye kuchoma.
آية رقم 12
Hakika malipizo ya Mola wako kwa maadui Zake na mateso Yake juu yao ni mazito.
آية رقم 13
Ndiye Yeye Mwenye kuanzisha kuumba na kisha kurudisha.
آية رقم 14
Ndiye Yeye Mwingi wa kusamehe kwa wenye kutubia, Mwingi wa mapenzi kwa wanaoikurubisha kwake.
آية رقم 16
Mfanya Alitakalo: hakuna kitu Anachotaka kiwe kisiwe.
آية رقم 17
Je, ewe Mtume, imekufikia habari ya makundi yaliyokufuru na kukanusha Mitume walioletwa, ya
آية رقم 18
Firauni na Thamūd, misiba na adhabu iliyowashukia? Hawakuzingatia kwa habari hiyo.
آية رقم 19
Bali waliokufuru waendelea kukanusha kwao, kama walivyokuwa waliokuja kabla yao.
آية رقم 20
Na Mwenyezi Mungu Amewazunguka kwa Ujuzi na Uweza Wake, hakuna chenye kufichika Kwake kuhusu wao na vitendo vyao. Hii Qu’ani siyo kama wanavyodai wenye kukanusha katika washirikina kuwa ni mashairi na uchawi ndipo wakaikanusha.
آية رقم 22
iliyomo kwenye Ubao Uliohifadhiwa, haufikiwi na kubadilishwa wala kupotoshwa.
تقدم القراءة