ترجمة معاني سورة الغاشية باللغة السواحلية من كتاب Ali Muhsin Al - Swahili translation
ﰡ
آية رقم 1
ﭽﭾﭿﮀ
ﮁ
Al-Ghashiyah
Je! Imekufikia khabari ya msiba wa kufudikiza?
آية رقم 2
ﮂﮃﮄ
ﮅ
Siku hiyo nyuso zitainama,
آية رقم 3
ﮆﮇ
ﮈ
Zikifanya kazi, nazo taabani.
آية رقم 4
ﮉﮊﮋ
ﮌ
Ziingie katika Moto unao waka -
آية رقم 5
ﮍﮎﮏﮐ
ﮑ
Zikinyweshwa kutoka chemchem inayo chemka.
آية رقم 6
ﮒﮓﮔﮕﮖﮗ
ﮘ
Hawatakuwa na chakula isipo kuwa kichungu chenye miba.
آية رقم 7
ﮙﮚﮛﮜﮝﮞ
ﮟ
Hakinenepeshi wala hakiondoi njaa.
آية رقم 8
ﮠﮡﮢ
ﮣ
Siku hiyo nyuso nyengine zitakuwa kunjufu.
آية رقم 9
ﮤﮥ
ﮦ
Zitakuwa radhi kwa juhudi yao,
آية رقم 10
ﮧﮨﮩ
ﮪ
Katika Bustani ya juu.
آية رقم 11
ﮫﮬﮭﮮ
ﮯ
Hawatasikia humo upuuzi.
آية رقم 12
ﮰﮱﯓ
ﯔ
Humo imo chemchem inayo miminika.
آية رقم 13
ﯕﯖﯗ
ﯘ
Humo vimo viti vilivyo nyanyuliwa,
آية رقم 14
ﯙﯚ
ﯛ
Na bilauri zilizo pangwa,
آية رقم 15
ﯜﯝ
ﯞ
Na matakia safu safu,
آية رقم 16
ﯟﯠ
ﯡ
Na mazulia yaliyo tandikwa.
آية رقم 17
ﯢﯣﯤﯥﯦﯧ
ﯨ
Je! Hawamtazami ngamia jinsi alivyo umbwa?
آية رقم 18
ﯩﯪﯫﯬ
ﯭ
Na mbingu jinsi ilivyo inuliwa?
آية رقم 19
ﯮﯯﯰﯱ
ﯲ
Na milima jinsi ilivyo thibitishwa?
آية رقم 20
ﯳﯴﯵﯶ
ﯷ
Na ardhi jinsi ilivyo tandazwa?
آية رقم 21
ﯸﯹﯺﯻ
ﯼ
Basi kumbusha! Hakika wewe ni Mkumbushaji.
آية رقم 22
ﯽﯾﯿ
ﰀ
Wewe si mwenye kuwatawalia.
آية رقم 23
ﭑﭒﭓﭔ
ﭕ
Lakini anaye rudi nyuma na kukataa,
آية رقم 24
ﭖﭗﭘﭙ
ﭚ
Basi Mwenyezi Mungu atamuadhibu kwa adhabu iliyo kubwa kabisa!
آية رقم 25
ﭛﭜﭝ
ﭞ
Hakika ni kwetu Sisi ndio marejeo yao.
آية رقم 26
ﭟﭠﭡﭢ
ﭣ
Kisha hakika ni juu yetu Sisi hisabu yao!
تقدم القراءة