ترجمة معاني سورة ق باللغة السواحلية من كتاب Ali Muhsin Al - Swahili translation
ﰡ
آية رقم 1
ﭑﭒﭓﭔ
ﭕ
Kaaf
Qaaf. Naapa kwa Qur'ani tukufu!
آية رقم 2
Bali wanastaajabu kwamba amewafikia mwonyaji kutoka miongoni mwao, na wakasema makafiri: Hili ni jambo la ajabu!
آية رقم 3
Ati tukifa na tukawa udongo...? Kurejea huko kuko mbali!
آية رقم 4
Hakika Sisi tunajua kiasi cha kila kinacho punguzwa na ardhi kutokana nao. Na kwetu kipo Kitabu kinacho hifadhi yote.
آية رقم 5
Lakini waliikanusha Haki ilipo wajia; kwa hivyo wamo katika mambo ya mkorogo.
آية رقم 6
Je! Hawaangalii mbingu zilizo juu yao! Vipi tulivyo zijenga, na tukazipamba. Wala hazina nyufa.
آية رقم 7
Na ardhi tumeitandaza na tukaiwekea milima, na tukaiotesha mimea mizuri ya kila namna.
آية رقم 8
ﮙﮚﮛﮜﮝ
ﮞ
Yawe haya ni kifumbua macho na ukumbusho kwa kila mja mwenye kuelekea.
آية رقم 9
Na tumeteremsha kutoka mbinguni maji yaliyo barikiwa, na kwa hayo tukaotesha mabustani na nafaka za kuvunwa.
آية رقم 10
ﮪﮫﮬﮭﮮ
ﮯ
Na mitende mirefu yenye makole yaliyo zaa kwa wingi,
آية رقم 11
Ili iwe ni riziki kwa waja wangu. Na tukaifufua kwa maji nchi iliyo kuwa imekufa. Kama hivyo ndivyo utakavyo kuwa ufufuaji.
آية رقم 12
Kabla yao walikadhibisha kaumu ya Nuhu na wakaazi wa Rassi na Thamudi.
آية رقم 13
ﯤﯥﯦﯧ
ﯨ
Na A'di na Firauni na kaumu ya Lut'i.
آية رقم 14
Na wakaazi wa Machakani, na watu wa Tubbaa'. Wote hao waliwakanusha Mitume, kwa hivyo onyo likathibitika juu yao.
آية رقم 15
Kwani tulichoka kwa kuumba mara ya kwanza. Bali wao wamo katika shaka tu juu ya umbo jipya.
آية رقم 16
Na hakika tumemuumba mtu, nasi tunayajua yanayo mpitikia katika nafsi yake. Na Sisi tuko karibu naye kuliko mshipa wa shingoni mwake.
آية رقم 17
Wanapo pokea wapokeaji wawili, wanao kaa kuliani na kushotoni.
آية رقم 18
Hatamki neno ila karibu yake yupo mwangalizi tayari.
آية رقم 19
Na uchungu wa kutoka roho utamjia kwa haki. Hayo ndiyo uliyo kuwa ukiyakimbia.
آية رقم 20
Na litapulizwa baragumu. Hiyo ndiyo Siku ya Miadi.
آية رقم 21
ﮆﮇﮈﮉﮊﮋ
ﮌ
Na kila nafsi itakuja na pamoja nayo mchungaji na shahidi.
آية رقم 22
(Aambiwe): Kwa hakika ulikuwa umeghafilika na haya; basi leo tumekuondolea pazia lako, na kwa hivyo kuona kwako leo ni kukali.
آية رقم 23
ﮚﮛﮜﮝﮞﮟ
ﮠ
Na mwenzake atasema: Huyu niliye naye mimi kesha tayarishwa.
آية رقم 24
ﮡﮢﮣﮤﮥﮦ
ﮧ
Mtupeni katika Jahannamu kila kafiri mwenye inda,
آية رقم 25
ﮨﮩﮪﮫ
ﮬ
Akatazaye kheri, arukaye mipaka, mwenye kutia shaka,
آية رقم 26
Aliye weka mungu mwengine pamoja na Mwenyezi Mungu. Basi mtupeni katika adhabu kali.
آية رقم 27
Mwenzake aseme: Ee Mola wetu Mlezi! Sikumpoteza mimi, bali yeye mwenyewe alikuwa katika upotovu wa mbali.
آية رقم 28
(Mwenyezi Mungu) aseme: Msigombane mbele yangu. Nilikuleteeni mbele onyo langu.
آية رقم 29
Mbele yangu haibadilishwi kauli, wala Mimi siwadhulumu waja wangu.
آية رقم 30
Siku tutapo iambia Jahannamu: Je! Umejaa? Nayo itasema: Je! Kuna ziada?
آية رقم 31
ﰁﰂﰃﰄﰅ
ﰆ
Na Pepo italetwa karibu kwa ajili ya wachamngu, haitakuwa mbali.
آية رقم 32
ﰇﰈﰉﰊﰋﰌ
ﰍ
Haya ndiyo mnayo ahidiwa kwa kila mwenye kurejea kwa Mwenyezi Mungu na akajilinda.
آية رقم 33
Mwenye kumwogopa Mwingi wa Rehema hali kuwa hamwoni, na akaja kwa moyo ulio elekea-
آية رقم 34
ﰖﰗﰘﰙﰚﰛ
ﰜ
(Ataambiwa) ingieni kwa salama. Hiyo ndiyo siku ya daima dawamu.
آية رقم 35
ﰝﰞﰟﰠﰡﰢ
ﰣ
Humo watapata wakitakacho, na kwetu yako ya ziada.
آية رقم 36
Na kaumu ngapi tuliziangamiza kabla yao walio kuwa na nguvu zaidi kuliko hawa! Nao walitanga tanga katika nchi nyingi. Je! Walipata pa kukimbilia?
آية رقم 37
Hakika katika hayo upo ukumbusho kwa mwenye moyo au akatega sikio naye yupo anashuhudia.
آية رقم 38
Na bila ya shaka Sisi tumeziumba mbingu na ardhi na vilio baina yao mnamo siku sita; na wala hayakutugusa machofu.
آية رقم 39
Basi vumilia kwa hayo wasemayo, na mtakase kwa kumsifu Mola wako Mlezi kabla ya kuchomoza jua na kabla ya kuchwa.
آية رقم 40
ﮊﮋﮌﮍﮎ
ﮏ
Na katika usiku pia mtakase, na baada ya kusujudu.
آية رقم 41
Na sikiliza siku atapo nadi mwenye kunadi kutoka pahala karibu.
آية رقم 42
Siku watakapo sikia ukelele wa haki. Hiyo ndiyo siku ya kufufuka.
آية رقم 43
ﮡﮢﮣﮤﮥﮦ
ﮧ
Hakika Sisi tunahuisha na tunafisha, na kwetu Sisi ndio marejeo.
آية رقم 44
Siku itapo wapasukia ardhi mbio mbio! Mkusanyo huo kwetu ni mwepesi.
آية رقم 45
Sisi tunajua kabisa wayasemayo. Wala wewe si mwenye kuwatawalia kwa ujabari. Basi mkumbushe kwa Qur'ani anaye liogopa onyo.
تقدم القراءة