ترجمة سورة الهمزة

Ali Muhsin Al - Swahili translation
ترجمة معاني سورة الهمزة باللغة السواحلية من كتاب Ali Muhsin Al - Swahili translation .

Ali-Humazah


Ole wake kila safihi, msengenyaji!

Aliye kusanya mali na kuyahisabu.

Anadhani ya kuwa mali yake yatambakisha milele!

Hasha! Atavurumishwa katika H'ut'ama.

Na nani atakujuvya ni nini H'ut'ama?

Moto wa Mwenyezi Mungu ulio washwa.

Ambao unapanda nyoyoni.

Hakika huo utafungiwa nao

Kwenye nguzo zilio nyooshwa.
Icon