ترجمة معاني سورة الأعلى باللغة السواحلية من كتاب Ali Muhsin Al - Swahili translation
ﰡ
آية رقم 1
ﮟﮠﮡﮢ
ﮣ
Al'A'alah
Litakase jina la Mola wako Mlezi aliye juu kabisa,
آية رقم 2
ﮤﮥﮦ
ﮧ
Aliye umba, na akaweka sawa,
آية رقم 3
ﮨﮩﮪ
ﮫ
Na ambaye amekadiria na akaongoa,
آية رقم 4
ﮬﮭﮮ
ﮯ
Na aliye otesha malisho,
آية رقم 5
ﮰﮱﯓ
ﯔ
Kisha akayafanya makavu, meusi.
آية رقم 6
ﯕﯖﯗ
ﯘ
Tutakusomesha wala hutasahau,
آية رقم 7
Ila akipenda Mwenyezi Mungu. Hakika Yeye anayajua yaliyo dhaahiri na yaliyo fichikana.
آية رقم 8
ﯤﯥ
ﯦ
Na tutakusahilishia yawe mepesi.
آية رقم 9
ﯧﯨﯩﯪ
ﯫ
Basi kumbusha, kama kukumbusha kunafaa.
آية رقم 10
ﯬﯭﯮ
ﯯ
Atakumbuka mwenye kuogopa.
آية رقم 11
ﭑﭒ
ﭓ
Na atajitenga mbali nayo mpotovu,
آية رقم 12
ﭔﭕﭖﭗ
ﭘ
Ambaye atauingia Moto mkubwa.
آية رقم 13
ﭙﭚﭛﭜﭝﭞ
ﭟ
Tena humo hatakufa wala hawi hai.
آية رقم 14
ﭠﭡﭢﭣ
ﭤ
Hakika amekwisha fanikiwa aliye jitakasa.
آية رقم 15
ﭥﭦﭧﭨ
ﭩ
Na akakumbuka jina la Mola wake Mlezi, na akasali.
آية رقم 16
ﭪﭫﭬﭭ
ﭮ
Lakini nyinyi mnakhiari maisha ya dunia!
آية رقم 17
ﭯﭰﭱ
ﭲ
Na Akhera ni bora na yenye kudumu zaidi.
آية رقم 18
ﭳﭴﭵﭶﭷ
ﭸ
Hakika haya yamo katika Vitabu vya mwanzo,
آية رقم 19
ﭹﭺﭻ
ﭼ
Vitabu vya Ibrahimu na Musa.
تقدم القراءة