فَلَا تَكُ فِي مِرۡيَةٖ مِّمَّا يَعۡبُدُ هَـٰٓؤُلَآءِۚ مَا يَعۡبُدُونَ إِلَّا كَمَا يَعۡبُدُ ءَابَآؤُهُم مِّن قَبۡلُۚ وَإِنَّا لَمُوَفُّوهُمۡ نَصِيبَهُمۡ غَيۡرَ مَنقُوصٖ
Basi usiwe na shaka juu ya wanayo yaabudu hao. Hawaabudu ila kama walivyo abudu baba zao zamani. Na hakika Sisi tutawatimilizia fungu lao bila ya kupunguzwa.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Basi usiwe, ewe Mtume, katika shaka kuhusu ubatilifu wa vitu wanavyoviabudu washirikina hawa miongoni mwa watu wako. Wao hawaabudu, miongoni mwa masanamu, isipokuwa kama vile baba zao walikuwa wakiabudu huko nyuma. Na sisi ni wenye kuwatekelezea kile tulichowaahidi kikiwa kikamilifu kisichopunguzwa. Huu ni muelekezo kwa ummah wote, ingawa tamko lake limeelekezwa kwa Mtume, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani ziwashukie.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس