أُوْلَـٰٓئِكَ لَمۡ يَكُونُواْ مُعۡجِزِينَ فِي ٱلۡأَرۡضِ وَمَا كَانَ لَهُم مِّن دُونِ ٱللَّهِ مِنۡ أَوۡلِيَآءَۘ يُضَٰعَفُ لَهُمُ ٱلۡعَذَابُۚ مَا كَانُواْ يَسۡتَطِيعُونَ ٱلسَّمۡعَ وَمَا كَانُواْ يُبۡصِرُونَ
Hao hawawezi kushinda katika ardhi, wala hawana walinzi isipo kuwa Mwenyezi Mungu. Watazidishiwa adhabu. Hawakuwa wakiweza kusikia wala hawakuwa wakiona.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Makafiri hao hawakuwa ni wenye kumhepa Mwenyezi Mungu kwa kumkimbia, na hawakuwa na wasaidizi wa kuwazuia wao wasipata mateso ya Mwenyezi Mungu. Wataongezewa adhabu katika Jahanamu, kwa kuwa wao walikuwa hawawezi kuisikia Qur’ani kwa namna ya kuwafanya wanufaike au wazione alama za Mwenyezi Mungu katika ulimwengu kwa namana ya kuwafanya waongoke, kwani wao walikuwa wameshughulika na ukafiri ambao walikuwa wamedumu nao.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس