قَالَ إِنَّمَا يَأۡتِيكُم بِهِ ٱللَّهُ إِن شَآءَ وَمَآ أَنتُم بِمُعۡجِزِينَ
Akasema: Mwenyezi Mungu atakuleteeni akipenda. Wala nyinyi si wenye kumshinda.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Nūḥ, akasema kuwaambia watu wake, «Mwenyezi Mungu , Peke Yake, Ndiye Atakayewaletea nyinyi adhabu atakapo, na nyinyi si wenye kuiponyoka Akitaka kuwaadhibu, kwani Yeye, kutakata na sifa za upungufu ni Kwake, hakuna chochote chenye kumlemea katika ardhi wala katika mbingu.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس