يَٰقَوۡمِ لَآ أَسۡـَٔلُكُمۡ عَلَيۡهِ أَجۡرًاۖ إِنۡ أَجۡرِيَ إِلَّا عَلَى ٱلَّذِي فَطَرَنِيٓۚ أَفَلَا تَعۡقِلُونَ
Enyi watu wangu! Sikuombeni ujira kwa ajili ya haya. Haukuwa ujira wangu ila kwa Yule aliye niumba. Basi hamtumii akili?
Ali Muhsin Al - Swahili translation
«Enyi watu wangu, mimi siwaombi malipo yoyote, kwa haya niwalinganiyao ya kumtakasia Mwenyezi Mungu ibada na kuacha kuabudu masanamu,. Malipo yangu mimi ya kuwalingania nyinyi hayako juu ya yoyote isipokuwa Mwenyezi Mungu aliyeniumba. Basi hamtii akili mkatenganisha baina ya ukweli na upotofu?
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس