وَأَخَذَ ٱلَّذِينَ ظَلَمُواْ ٱلصَّيۡحَةُ فَأَصۡبَحُواْ فِي دِيَٰرِهِمۡ جَٰثِمِينَ
Na ukelele uliwaangamiza wale walio dhulumu, wakapambazukiwa nao ni maiti majumbani mwao.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na ukelele wa nguvu uliwapata Thamūd walio madhalimu, hapohapo wakawa kwenye majumba yao ni wafu waliokauka na kuanguka kwa nyuso zao, hakuna anayetikisika.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس