وَيَٰقَوۡمِ لَا يَجۡرِمَنَّكُمۡ شِقَاقِيٓ أَن يُصِيبَكُم مِّثۡلُ مَآ أَصَابَ قَوۡمَ نُوحٍ أَوۡ قَوۡمَ هُودٍ أَوۡ قَوۡمَ صَٰلِحٖۚ وَمَا قَوۡمُ لُوطٖ مِّنكُم بِبَعِيدٖ
Na enyi watu wangu! Kukhalifiana nami kusikupelekeeni hata mkasibiwa kama walivyo sibiwa watu wa Nuhu, au watu wa Hud, au watu wa Saleh. Na watu wa Lut' si mbali nanyi.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
«Na enyi watu wangu, usiwapelekee uadui wenu kwangu na kunichukia na kuiacha Dini niliyonayo, kufanya ukakamavu na kuendelea na ukanushaji wa Mwenyezi Mungu mlionao. Kwani mkifanya hivyo, yatawapata nyinyi maangamivu kama yaliyowapata watu wa Nūḥ, au watu wa Hūd au watu wa Ṣāliḥ,. Na hawakuwa watu wa Lūṭ, na adhabu iliyowashukia ni mbali na nyinyi, si nchi waliyoishi wala zama walizokuwako.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس