إِلَىٰ فِرۡعَوۡنَ وَمَلَإِيْهِۦ فَٱتَّبَعُوٓاْ أَمۡرَ فِرۡعَوۡنَۖ وَمَآ أَمۡرُ فِرۡعَوۡنَ بِرَشِيدٖ
Kwa Firauni na waheshimiwa wake. Lakini wao walifuata amri ya Firauni, na amri ya Firauni haikuwa yenye uwongofu.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Tulimtuma Mūsā kwa Fir'awn na wakubwa wa wafuasi wake na watukufu wa watu wake, Fir'awn akakanusha na akawaamuru watu wake wamfuate yeye, wakamtii yeye na wakaenda kinyume cha amri ya Mūsā. Na hakuna uongofu wowote wala muongozo mwema katika amri ya Fir'awn, ni ujinga mtupu, upotevu, ukanushaji na ujeuri.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس