وَءَاتِ ذَا ٱلۡقُرۡبَىٰ حَقَّهُۥ وَٱلۡمِسۡكِينَ وَٱبۡنَ ٱلسَّبِيلِ وَلَا تُبَذِّرۡ تَبۡذِيرًا
Na mpe aliye jamaa yako haki yake, na masikini, na msafiri; wala usitumie ovyo kwa fujo.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na umfanyie wema kila mwenye ukaribu wa ujamaa na wewe, na umpe haki yake ya wema na hisani, na umpe masikini mwenye uhitaji na msafiri aliyeepukana na watu wake na mali yake, na usitumie mali yako katika njia isiyokuwa ya kumtii Mwenyezi Mungu au kwa njia ya kupita kiasi na ufujaji.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس