إِنَّ ٱلۡمُبَذِّرِينَ كَانُوٓاْ إِخۡوَٰنَ ٱلشَّيَٰطِينِۖ وَكَانَ ٱلشَّيۡطَٰنُ لِرَبِّهِۦ كَفُورٗا
Hakika wabadhirifu ni ndugu wa Mashet'ani. Na Shet'ani ni mwenye kumkufuru Mola wake Mlezi.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Hakika wale wenye kupita kiasi katika matumizi na wenye kutoa mali yao katika kumuasi Mwenyezi Mungu wanafanana na Mashetani kwenye uovu, uharibifu na maasia, na Shetani ni mwingi wa kukufuru, ni mkanushaji sana neema za Mola wake.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس