وَلَا تَقۡتُلُوٓاْ أَوۡلَٰدَكُمۡ خَشۡيَةَ إِمۡلَٰقٖۖ نَّحۡنُ نَرۡزُقُهُمۡ وَإِيَّاكُمۡۚ إِنَّ قَتۡلَهُمۡ كَانَ خِطۡـٔٗا كَبِيرٗا
Wala msiwauwe wana wenu kwa kuogopa umasikini. Sisi tunawaruzuku wao na nyinyi. Hakika kuwaua hao ni khatia kubwa.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na mkijua kwamba riziki iko kwenye mkono wa Mwenyezi Mungu, kutkata na sifa za upungufu ni Kwake, basi msiwaue watoto wenu kwa kuchelea umasikini, kwani Yeye, kutakata na sifa za upungufu ni Kwake, Ndiye Mwenye kuwaruzuku waja Wake, Anawruzuku wana kama Anavyowaruzuku wazazi. Hakika kuua watoto ni dhambi kubwa.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس