قُل لَّوۡ كَانَ مَعَهُۥٓ ءَالِهَةٞ كَمَا يَقُولُونَ إِذٗا لَّٱبۡتَغَوۡاْ إِلَىٰ ذِي ٱلۡعَرۡشِ سَبِيلٗا
Sema: Lau kuwa wangeli kuwa pamoja naye miungu mingine kama wasemavyo, basi wangeli tafuta njia ya kumfikia Mwenye Kiti cha Enzi.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Sema, ewe Mtume, kuwaambia washirikina, «Lau kulikuwa na waungu wengine pamoja na Mwenyezi Mungu, basi wangalitafuta waungu hao njia ya kushindana na Mwenyezi Mungu Mwenye 'Arshi iliyo kubwa.»
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس