قَالَ ٱذۡهَبۡ فَمَن تَبِعَكَ مِنۡهُمۡ فَإِنَّ جَهَنَّمَ جَزَآؤُكُمۡ جَزَآءٗ مَّوۡفُورٗا
Akasema Mwenyezi Mungu: Ondokelea mbali! Atakaye kufuata katika wao, basi Jahannamu itakuwa ndiyo malipo yenu, malipo ya kutimia.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Mwenyezi Mungu Aliyetukuka Akasema Akimuonya Iblisi na wafuasi wake, «Enda! Yoyote mwenye kukufuata miongoni mwa kizazi cha Ādam, basi mateso yako na mateso yao ndani ya moto wa Jahanamu ni mengi.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس