وَقَالُواْ لَن نُّؤۡمِنَ لَكَ حَتَّىٰ تَفۡجُرَ لَنَا مِنَ ٱلۡأَرۡضِ يَنۢبُوعًا
Na walisema: Hatutakuamini mpaka ututimbulie chemchem katika ardhi hii.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na Qur’ani ilipowaelemea washirikina na ikawashinda, waliingia kutaka miujiza kulingana na mapendeleo yao wakasema, «Hatutakuamini, ewe Muhammad, na hatutafanya vile unavyosema mpaka utupasulie kwenye ardhi ya Makkah chemchemu ya maji yenye kupita.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس