ٱلۡمُلۡكُ يَوۡمَئِذٍ ٱلۡحَقُّ لِلرَّحۡمَٰنِۚ وَكَانَ يَوۡمًا عَلَى ٱلۡكَٰفِرِينَ عَسِيرٗا
Ufalme wa haki siku hiyo utakuwa wa Arrahman, Mwingi wa Rehema, na itakuwa siku ngumu kwa makafiri.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Mamlaka ya kikweli katika Siku hii ni ya Mwingi wa rehema Peke Yake bila mwingine. Na Siku hii itakuwa ngumu kwa makafiri kwa mateso yatakayowapata na adhabu kali.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس