وَيَوۡمَ يَعَضُّ ٱلظَّالِمُ عَلَىٰ يَدَيۡهِ يَقُولُ يَٰلَيۡتَنِي ٱتَّخَذۡتُ مَعَ ٱلرَّسُولِ سَبِيلٗا
Na siku ambayo mwenye kudhulumu atajiuma mikono yake, na huku anasema: Laiti ningeli shika njia pamoja na Mtume!
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na ikumbuke, ewe Mtume, Siku ambayo mwenye kujidhulumu nafsi yake ataiuma mikono yake kwa majuto na unguliko kwa kusema, «Laiti mimi niliandamana na Mtume wa Mwenyezi Mungu Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, na nikamfuata katika kuufanya Uislamu kuwa ni njia ya Peponi,»
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس