أَرَءَيۡتَ مَنِ ٱتَّخَذَ إِلَٰهَهُۥ هَوَىٰهُ أَفَأَنتَ تَكُونُ عَلَيۡهِ وَكِيلًا
Je! Umemwona aliye yafanya matamanio yake kuwa ndio mungu wake? Basi je, wewe utakuwa ni wakili wake?
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Mwangalie, ewe Mtume, kwa kumuonea ajabu yule aliyeyatii matamanio yake kama kumtii Mwenyezi Mungu. Je, wewe utakuwa ni mwenye kumtunza mpaka umrudishe kwenye Imani?
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس