أَوۡ يُلۡقَىٰٓ إِلَيۡهِ كَنزٌ أَوۡ تَكُونُ لَهُۥ جَنَّةٞ يَأۡكُلُ مِنۡهَاۚ وَقَالَ ٱلظَّـٰلِمُونَ إِن تَتَّبِعُونَ إِلَّا رَجُلٗا مَّسۡحُورًا
Au akaangushiwa khazina juu yake, au akawa na bustani ale katika hiyo? Wakasema madhaalimu: Nyinyi hamumfuati ila mtu aliye rogwa.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
au imshukie kutoka mbinguni kanzi ya mali, au awe na shamba kubwa ambalo yeye anakula matunda yake.» Na wakaendelea kusema, hawa madhalimu wenye kukanusha, «Mumfuatao nyinyi si mwingine isipokuwa ni mtu aliyefanyiwa uchawi ulioathiri akili yake.»
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس