بَلۡ بَدَا لَهُم مَّا كَانُواْ يُخۡفُونَ مِن قَبۡلُۖ وَلَوۡ رُدُّواْ لَعَادُواْ لِمَا نُهُواْ عَنۡهُ وَإِنَّهُمۡ لَكَٰذِبُونَ
Bali yamewadhihirikia waliyo kuwa wakiyaficha zamani. Na kama wangeli rudishwa bila ya shaka wange yarejea yale yale waliyo katazwa. Na hakika hao ni waongo.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Mambo si kama hivyo! Bali Siku ya Kiyama yatawadhihirikia wao yale waliokuwa wakiyafanya kwa nafsi zao, ya kuamini ukweli wa yale ambayo Mitume walikuja nayo ulimwenguni, ingawa walikuwa wakiwadhihirishia wafuasi wao kinyume chake. Na lau ilikadiriwa warudishwe ulimwenguni na waongezewe muda, wangalirudi kwenye upinzani kwa kukufuru na kukanusha. Na kwa kweli wao ni warongo katika neno lao, «Lau tutarudishwa ulimwenguni hatungalizikanusha aya za Mola wetu na tungalikuwa Waumini.»
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس