۞وَأَمَّا ٱلَّذِينَ سُعِدُواْ فَفِي ٱلۡجَنَّةِ خَٰلِدِينَ فِيهَا مَا دَامَتِ ٱلسَّمَٰوَٰتُ وَٱلۡأَرۡضُ إِلَّا مَا شَآءَ رَبُّكَۖ عَطَآءً غَيۡرَ مَجۡذُوذٖ
Na ama wale walio bahatika, wao watakuwamo Peponi wakidumu humo muda wa kudumu mbingu na ardhi, isipo kuwa apendavyo Mola wako Mlezi. Hicho ni kipawa kisio na ukomo.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na ama wale ambao Mwenyezi Mungu Amewaruzuku wema, wataingia Peponi wakae milele humo muda wa kuwako mbingu na ardhi, isipokuwa lile kundi ambalo Mwenyezi Mungu Atataka kulichelewesha, nalo ni lile la waliompwekesha Mwenyezi Mungu waliofanya maasia. Wao watasalia Motoni kwa kipindi fulani, kisha watatoka humo kwenda Peponi kwa matakwa ya Mwenyezi Mungu na rehema Yake. Na Mwenyezi Mungu Atawapa watu wema hawa vipaji visizopunguzwa.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس