إِلَّا ٱلَّذِينَ صَبَرُواْ وَعَمِلُواْ ٱلصَّـٰلِحَٰتِ أُوْلَـٰٓئِكَ لَهُم مَّغۡفِرَةٞ وَأَجۡرٞ كَبِيرٞ
Ila wale walio subiri wakatenda mema. Hao watapata msamaha na ujira mkubwa.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Lakini wale waliosubiri juu ya yaliyowapata ya shida kwa kumuamini Mwenyezi Mungu na kutaka malipo kutoka Kwake, wakafanya mema kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa neema Zake, wao watakuwa na msamaha wa dhambi zao na malipo makubwa Akhera.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس