وَقُل لِّلَّذِينَ لَا يُؤۡمِنُونَ ٱعۡمَلُواْ عَلَىٰ مَكَانَتِكُمۡ إِنَّا عَٰمِلُونَ
Na waambie wale wasio amini: Fanyeni muwezavyo, nasi pia tunafanya.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Waambie, ewe Mtume, makafiri wasiokubali upweke wa Mwenyezi Mungu, «Fanyeni mnayoyafanya kwa namna yenu na mbinu zenu za kuupinga Ulinganizi na kumkera Mtume na wale waliomuitika, kwani sisi ni wenye kufanya kwa namna yetu mbinu zetu za kusimama imara juu ya Dini yetu na kutekeleza amri ya Mwenyezi Mungu.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس