وَلَئِنۡ أَذَقۡنَا ٱلۡإِنسَٰنَ مِنَّا رَحۡمَةٗ ثُمَّ نَزَعۡنَٰهَا مِنۡهُ إِنَّهُۥ لَيَـُٔوسٞ كَفُورٞ
Na tukimwonjesha mtu rehema inayo toka kwetu, kisha tukamwondolea, hukata tamaa akakufuru.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na lau tutampa mwanadamu neema ya afya na amani na zisokuwa hizo kisha tukamuondolea, hakika yeye atakuwa ni mwenye kukata tamaa sana na rehema ya Mwenyezi Mungu, ni mkanushaji sana wa neema ambazo Mwenyezi Mungu Amemneemesha nazo.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس